Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tamati Inayokuja ya “Kitabu cha Vita vya Yehova”
    Mnara wa Mlinzi—1990 | Julai 1
    • 16 Nabii Isaya arejezea ubora wa jina hilo amtajapo Yehova kuwa “yule Mmoja anayefanya mkono Wake wenye upendezi uende kwenye kiganja cha kulia cha Musa; yule Mmoja anayegawanya maji kutoka mbele yao ili kufanya jina linalodumu kwa wakati usio dhahiri kwa ajili ya unafsi wake mwenyewe.” Naye akimwambia Yehova, asema hivi: “Hivyo wewe uliongoza watu wako ili ufanye jina lenye upendezi kwa ajili ya unafsi wako mwenyewe.” (Isaya 63:12-14, NW) Akimsihi Yehova atende tena kwa ajili ya watu wake, Danieli alisema naye kwa kumtaja kuwa “uliyewatoa watu wako hawa katika nchi ya Misri kwa mkono hodari, ukajipatia sifa, kama ilivyo leo.”—Danieli 9:15; Yeremia 32:20.

  • Tamati Inayokuja ya “Kitabu cha Vita vya Yehova”
    Mnara wa Mlinzi—1990 | Julai 1
    • 20. Mfalme Hezekia aliwaambia maneno gani watu wake waliotishwa ili wajipe moyo, na Mashahidi wa Yehova leo hujipa moyo kwa kutegemea maneno ya Mfalme gani aliye mkubwa kuliko Hezekia?

      20 Hata hivyo, hao wala umati mkubwa wa Wakristo wenye tumaini la kidunia ambao wametoka mataifa yote ili kujiunga nao katika ibada safi hawahitaji kuhofu tokeo la shambulio hilo. Wakati majeshi yenye kuogopesha ya Senakeribu yalipokuja dhidi ya Yerusalemu katika utawala wa Mfalme Hezekia, Waisraeli waliohatarishwa walipewa mwono wenye kitulizo juu ya hali hiyo wakati Mfalme Hezekia alipowaambia hivi: “Kwake upo mkono wa mwili; ila kwetu yupo BWANA [Yehova, NW], Mungu wetu, kutusaidia, na kutupigania mapigano yetu.” Tokeo lilikuwa kwamba ‘watu waliyategemea maneno ya Hezekia, mfalme wa Yuda.’ (2 Nyakati 32:8) Mashahidi wa Yehova wa leo, watishwapo na majeshi ya kitaifa ya mfumo wa ulimwengu huu, waweza kujipa moyo kwa maneno kama hayo kutoka kwa mfalme mkubwa kuliko Hezekia, Yesu Kristo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki