-
Kaa Katika Bonde La Yehova La UlinziMnara wa Mlinzi—2013 | Februari 15
-
-
8. (a) Katika Biblia, milima inaweza kufananisha nini? (b) Ule “mlima wa mizeituni” unafananisha nini?
8 Kwa kuwa Yerusalemu—‘lile jiji’—linafananisha Yerusalemu la mbinguni, basi ule “mlima wa mizeituni, ulioko mbele ya Yerusalemu,” lazima uwe wa mfano. Mlima huo unafananisha nini? Nao “utapasuliwa katikati” na kuwa milima miwili kwa njia gani? Kwa nini Yehova anaiita “milima yangu”? (Soma Zekaria 14:3-5.) Katika Biblia, milima inaweza kufananisha falme, au serikali. Baraka na ulinzi huhusianishwa pia na mlima wa Mungu. (Zab. 72:3; Isa. 25:6, 7) Kwa hiyo, mlima wa mizeituni ambapo Mungu anasimama upande wa mashariki wa Yerusalemu la kidunia unafananisha enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote, yaani, utawala wake mkuu zaidi.
-
-
Kaa Katika Bonde La Yehova La UlinziMnara wa Mlinzi—2013 | Februari 15
-
-
WAABUDU WA KWELI WAANZA KUKIMBILIA KATIKA BONDE HILO!
11, 12. (a) Kukimbilia katika bonde la mfano kulianza lini? (b) Ni nini kinachothibitisha kwamba mkono wenye nguvu wa Yehova unawalinda watu wake?
11 Yesu aliwaonya wafuasi wake hivi: “Mtachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.” (Mt. 24:9) Chuki hiyo imezidi kuongezeka katika siku za mwisho za mfumo huu wa mambo, hasa tangu mwaka wa 1914. Licha ya kwamba mabaki watiwa-mafuta walishambuliwa vikali na wapinzani wao wakati wa Vita vya Kwanza vya Ulimwengu, kikundi hicho cha watu waaminifu hakikuangamizwa kabisa. Katika mwaka wa 1919, waliachiliwa huru kutoka katika utumwa wa Babiloni Mkubwa—ile milki ya ulimwenguni pote ya dini ya uwongo. (Ufu. 11:11, 12)a Huo ndio wakati ambapo watu walianza kukimbilia katika lile bonde la milima ya Yehova.
12 Tangu mwaka wa 1919, lile bonde la Mungu la ulinzi linaendelea kuwalinda waabudu wa kweli duniani pote. Kwa makumi ya miaka, machapisho ya Biblia na huduma ya shambani ya Mashahidi wa Yehova imepigwa marufuku na kuwekewa vizuizi katika sehemu nyingi za ulimwengu. Katika nchi fulani, bado Mashahidi wako chini ya vizuizi vya aina hiyo. Mataifa hayatafaulu kamwe kufutilia mbali ibada ya kweli hata yakijaribu kadiri gani! Yehova ataendelea kuutumia mkono wake wenye nguvu kuwalinda watu wake.—Kum. 11:2.
13. Tufanye nini ili tubaki katika bonde la Yehova la ulinzi, na kwa nini ni muhimu sana tufanye hivyo sasa?
13 Tukishikamana na Yehova na kusimama imara katika kweli, yeye na Mwana wake, Yesu Kristo, watatimiza sehemu yao, na Mungu hataruhusu kitu au mtu yeyote ‘atunyakue kutoka mkononi Mwake.’ (Yoh. 10:28, 29) Yehova yuko tayari kutupatia msaada wowote ule tunaohitaji ili tuendelee kumtii akiwa Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote na kuendelea kuwa raia washikamanifu wa Ufalme wa Kimasihi. Ni lazima tubaki katika bonde la ulinzi, kwa kuwa bonde hilo litakuwa muhimu zaidi kwa waabudu wa kweli wakati wa dhiki kuu inayokaribia upesi.
-