-
Kitabu Cha Biblia Namba 38—Zekaria“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
12. Ni kitia-moyo na uhakikisho gani ambavyo vyatolewa kuhusu ujenzi wa hekalu?
12 Njozi ya tano: Kile kinara cha taa na mizeituni (4:1-14). Malaika aamsha Zekaria aone kinara-taa cha dhahabu kilicho na taa saba, ikiwako mizeituni miwili kando yacho. Yeye asikia neno hili la Yehova kwa Zerubabeli: ‘Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho ya Mungu.’ “Mlima mkubwa” utatandazwa mbele ya Zerubabeli, na jiwe la kuwekwa juu kwenye kichwa cha hekalu litaletwa kwa mpaazo wa sauti: “Lavutia kama nini! Lavutia kama nini!” (NW) Zerubabeli ameiweka misingi ya hekalu, na Zerubabeli atamaliza kazi ile. Vinara vile saba ni macho ya Yehova ambayo “yapiga mbio huko na huko duniani mwote.” (4:6, 7, 10) Ile mizeituni miwili ni wapakwa-mafuta wawili wa Yehova.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 38—Zekaria“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
23. Maandishi ya Zekaria yaimarishaje imani?
23 Wote wanaojifunza na kutafakari juu ya unabii wa Zekaria watanufaika kupata maarifa yenye kuimarisha imani. Mara zaidi ya 50 Zekaria avuta fikira kwenye ‘Yehova wa majeshi’ kuwa Anayepigania watu Wake na kuwalinda, akiwajaza uwezo kwa kulingana na uhitaji wao. Wakati upinzani kama mlima ulipotishia ukamilishaji wa ujenzi wa hekalu, Zekaria alijulisha hivi rasmi: “Hili ndilo neno la BWANA [Yehova, NW] kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema BWANA [Yehova, NW] wa majeshi. Nani wewe, Ee mlima mkubwa? Mbele ya Zerubabeli utakuwa nchi tambarare.” Hekalu lilikamilishwa kwa msaada wa roho ya Yehova. Vivyo hivyo leo, vipingamizi vitayeyuka vikikabiliwa kwa imani katika Yehova. Ni kama vile Yesu alivyowaambia wanafunzi wake: “Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.”—Zek. 4:6, 7; Mt. 17:20.
-