Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Maono ya Zekaria Yanavyokuhusu
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Oktoba
    • 16. (a) Zekaria anaona jambo gani lingine? (Tazama picha ya 3 mwanzoni mwa makala hii.) (b) Wale wanawake wenye mabawa wanapeleka wapi kile chombo cha efa?

      16 Kisha Zekaria anawaona wanawake wawili wenye mabawa yenye nguvu kama ya korongo. (Soma Zekaria 5:9-11.) Wanawake hao wanatofautiana kabisa na yule mwanamke aliye ndani ya chombo cha efa! Wao wanatumia mabawa yao yenye nguvu kushuka haraka na kukiinua kile chombo cha efa chenye yule mwanamke anayefananisha “Uovu.” Wanampeleka wapi? “Uovu” anapelekwa katika “nchi ya Shinari,” au Babiloni. Lakini kwa nini wanawake hao wanapeleka chombo hicho Babiloni?

      17, 18. (a) Kwa nini Shinari ndipo ‘mahali anapopaswa’ kupelekwa yule mwanamke “Uovu”? (b) Tunapaswa kuazimia kufanya nini kuhusu uovu?

      17 Kwa Waisraeli wa siku za Zekaria, eneo la Shinari lilikuwa mahali panapofaa kumpeleka Uovu. Katika siku hizo, Zekaria na Wayahudi wenzake walijua kwamba jiji la Babiloni lilikuwa mahali penye uovu. Wakiwa wamelelewa katika mazingira ya jiji hilo lenye mambo machafu na ibada ya sanamu, walihitaji kupambana kila siku ili kupinga roho ya ulimwengu huo wa kipagani. Ni wazi kwamba maono hayo yaliwaletea kitulizo kikubwa sana, yaani, uhakika wa kwamba Yehova angedumisha ibada yake ikiwa safi!

      18 Hata hivyo, maono hayo pia yaliwakumbusha Wayahudi jukumu lao la kudumisha ibada yao ikiwa safi. Uovu hauwezi na hautaruhusiwa kupenya na kukaa miongoni mwa watu wa Yehova. Baada ya Yehova kutuleta ndani ya tengenezo lake lililo safi, linalotupa ulinzi na kututunza kwa upendo, tuna wajibu wa kusaidia kudumisha usafi huo. Je, tunachochewa kudumisha usafi wa tengenezo letu? Uovu wa aina yoyote haustahili kuwepo katika paradiso yetu ya kiroho.

  • Jinsi Maono ya Zekaria Yanavyokuhusu
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Oktoba
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki