-
Wakati wa Kujaribu na KupepetaMnara wa Mlinzi—1987 | Juni 15
-
-
Wakati wa Kujaribu na Kupepeta
“Na ghafula Bwana wa kweli atakuja katika hekalu lake, ambaye ninyi watu mnamtafuta, na mjumbe wa agano . . . na lazima yeye akae kama msafishaji na mtakasaji.”—MALAKI 3:1, 3, NW.
-
-
Wakati wa Kujaribu na KupepetaMnara wa Mlinzi—1987 | Juni 15
-
-
3. Ni jambo gani lililohusika katika kazi ya kusafisha ya kale?
3 Lakini, kwanza, kwa nini Yehova anawaruhusu watu wake wapite katika wakati wa kujaribu na kupepeta? Akiwa yeye ‘anayejaribu mioyo,’ amekusudia kusafisha watu wake waliopangwa kitengenezo. (Mithali 17:3; Zaburi 66:10) Katika nyakati za Biblia kazi ya kusafisha ilitia ndani kutia moto madini kiasi cha kuyeyuka kisha kuondoa uchafu au takataka. Tunasoma hivi: “Asafishaye anatazama kazi hiyo, akiwa amesimama au ameketi, kwa juhudi nyingi mpaka . .. [iliyoyeyuka] madini inaonekana kama kioo chenye kung’ara sana, ikirudisha sura ya kila kitu kinachoizunguka; hata asafishaye, anapotazama rundo la madini, anaweza kujiona mwenyewe kama katika kioo cha kujiangalia, na hivyo anaweza kutoa uamuzi ulio sahihi sana kuhusu usafi wa madini hiyo. Ikiwa ameridhika, moto huo unaondolewa, na madini inaondolewa katika jiko; lakini akifikiri kwamba si safi, moto zaidi unaongezwa na kazi hiyo inarudiwa.” (Cyclopedia of Biblical, Theological, and Ecclesiastical Literature, cha J. McClintock na J. Strong) Dhahabu au fedha kama hiyo iliyosafishwa ilikuwa bora zaidi.—Linganisha Ufunuo 3:18.
4. Kwa sababu gani Yehova anaruhusu kujaribiwa na kupepetwa miongoni mwa watu wake?
4 Yehova anaruhusu kujaribiwa na kupepetwa ili asafishe, au kutakasa, watu wake, akiwasaidia warudishe mfano wake kwa njia iliyo sahihi zaidi. (Waefeso 5:1) Katika kazi ya kusafisha, yeye anaziondoa takataka kwa kuyaondolea mbali mafundisho na mazoea machafu. (Isaya 1:25) Yeye pia anapepeta kutoka miongoni mwa watu wake wale ambao wanakataa kunyenyekea chini ya kazi ya kusafisha na ambao ‘wanaleta kukwazika na watu wanaovunja sheria.’ Jambo hilo linaweka njia wazi kwa “wale wana wa ule ufalme,” Waisraeli wa kiroho, wang’ae kwa uangavu ili kwamba jamii ya kidunia pia ikusanywe na kushikamana nao kitengenezo ili ije kuokolewa.—Mathayo 13:38, 41, 43, NW; Wafilipi 2:15.
-
-
Wakati wa Kujaribu na KupepetaMnara wa Mlinzi—1987 | Juni 15
-
-
14. (a) Kwa sababu gani kusafishwa kwa hekalu na Yesu katika 30 W.K. kwa wazi kulikuwa ishara tu ya jambo ambalo lingekuja kutukia? (b) Hekalu lilisafishwa katika njia gani na lini kwa utimizo wa Malaki 3:1?
14 Katika masika ya 30 W.K., Yesu alikuja kwenye hekalu la Yehova katika Yerusalemu na akawafukuza wale ambao walikuwa wakilifanya “kuwa nyumba ya biashara.” (Yohana 2:13-16) Lakini jambo hilo lilikuwa tu ishara ya yale ambayo yangetukia kwa utimizo wa unabii wa Malaki. Kufuatia kisa hiki, Yohana, akiwa yule “mjumbe,” aliendelea kuwabatiza na kuwaelekeza wanafunzi wake kwa Yesu. (Yohana 3:23-30) Hata hivyo, katika Nisani 9, 33 W.K., Yesu aliingia kwa shangwe katika Yerusalemu, akijitokeza mwenyewe kuwa Mfalme. (Mathayo 21:1-9; Zekaria 9:9) Yohana alikuwa ameimaliza kazi yake, akiwa amekatwa kichwa na Herode karibu mwaka mmoja mbele. Hivyo wakati Yesu alipokuja kwenye hekalu katika Nisani 10, alikuja kwa njia rasmi akiwa “yule mjumbe wa agano,” akiwa mwakilishi wa kuhukumu wa yule “Bwana [wa kweli]” Yehova, kwa utimizo wa Malaki 3:1. Yesu alilisafisha hekalu, akiwafukuza wale ambao walikuwa wakifanya biashara humo, akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadili fedha. Yeye alizidi kusema: “Je! haikuandikwa [katika Isaya 56:7], Nyumba ya [Yehova] itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote? Bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.”—Marko 11:15-18.
15. Kama jamii, viongozi wa kidini wa Kiyahudi waliitikiaje kazi ya kusafisha, lakini ni jambo gani lililokuwa kweli kuhusu makuhani fulani?
15 Hivyo taarifa ilitolewa kwa viongozi wa kidini wa Israeli kwamba wakati wao ulikuwa umefika. Kama jamii, walikataa kumkubali “mjumbe wa agano” wa Yehova. Wao ‘hawakuistahimili siku ya kuja kwake’ kwa kuwa wao walikataa kutii kwa unyenyekevu kazi ya kusafisha ya Msafishaji Mkuu. (Malaki 3:2, 3) Walistahili kupepetwa kama wanaostahili uharibifu. Ingawaje, kwa wazi, kulikuwako na “wana wa Lawi” wengine wenye mioyo mizuri, kwa kuwa muda mfupi baada ya kifo cha Yesu “jamii kubwa ya makuhani [Walawi] wakaitii ile Imani.”—Matendo 6:7.
-