Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu Cha Biblia Namba 39—Malaki
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 3. Ni nini kinachoonyesha kwamba unabii wa Malaki uliandikwa baada ya 443 K.W.K.?

      3 Unabii huu uliandikwa wakati gani? Ilikuwa wakati wa usimamizi wa gliwali fulani, jambo ambalo lauweka katika wakati wa kurejeshwa kwa Yerusalemu kufuatia ukiwa wa Yuda wa miaka 70. (Mal. 1:8) Lakini liwali yupi? Kwa kuwa utumishi wa hekaluni watajwa lakini bila kurejezea ujenzi wa hekalu, lazima iwe ilikuwa baada ya wakati wa Liwali Zerubabeli, ambaye hekalu lilikamilishwa wakati wa kuwa kwake ofisini. Kuna liwali mwingine mmoja tu wa kipindi hicho anayetajwa katika Maandiko, naye ni Nehemia. Je! unabii huu unalingana na wakati wa Nehemia? Hakuna linalotaarifiwa katika Malaki kuhusu kujengwa upya kwa Yerusalemu na ukuta walo, hiyo ikifanya sehemu ya mapema ya uliwali wa Nehemia iwe haihusiki hata kidogo. Hata hivyo, mengi yasemwa juu ya matumizi mabaya ya ukuhani, hiyo ikiunganisha Malaki na hali iliyokuwako wakati Nehemia alipokuja Yerusalemu mara ya pili, kufuatia kuitwa kwake tena na Artashasta aende Babuloni katika 443 K.W.K., mwaka wa 32 wa utawala wa mfalme huyo. (Mal. 2:1; Neh. 13:6) Vifungu vinavyofanana na hicho katika Malaki na Nehemia vyaonyesha kwamba unabii huu watumika kuhusu wakati huo hasa.—Mal. 2:4-8, 11, 12—Neh. 13:11, 15, 23-26; Mal. 3:8-10—Neh. 13:10-12.

  • Kitabu Cha Biblia Namba 39—Malaki
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 8. Ni jinsi gani makuhani wametia unajisi meza ya Yehova, na kwa nini laana itakuja juu yao?

      8 Sasa Yehova aelekeza maneno moja kwa moja kwa ‘makuhani wanaolidharau jina lake.’ Wanapojaribu kujitetea kuwa wenye haki, Yehova aelekeza kwenye dhabihu zao za upofu, ulema, na ugonjwa, naye auliza, Je! hata liwali atakubalia matoleo kama hayo? Yehova mwenyewe hana upendezo nayo. Lazima jina lake likwezwe miongoni mwa mataifa, lakini watu hawa wamtia unajisi kwa kusema: “Meza ya BWANA [Yehova, NW] imetiwa unajisi.” Laana itakuja juu yao kwa sababu wao wametumia ujanja kuepa nadhiri zao ili wasitoe dhabihu zinazostahiki. “Kwa maana mimi ni Mfalme mkuu, asema BWANA [Yehova, NW] wa majeshi, na jina langu [litakuwa, NW] latisha katika Mataifa.”—1:6, 12, 14.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki