Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ni Nani Atakayeokoka Siku ya Yehova?
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Mei 1
    • Ni Nani Atakayeokoka Siku ya Yehova?

      “Siku ile inakuja, inawaka kama tanuru.”—MALAKI 4:1.

      1. Malaki anafafanuaje mwisho wa mfumo huu mwovu?

      NABII Malaki alipuliziwa na Mungu kuandika unabii unaohusu mambo yenye kutisha yatakayotokea hivi karibuni. Mambo hayo yataathiri kila mtu duniani. Andiko la Malaki 4:1 linatabiri hivi: “Angalieni, siku ile inakuja, inawaka kama tanuru; na watu wote wenye kiburi, nao wote watendao uovu, watakuwa makapi; na siku ile inayokuja itawateketeza, asema BWANA wa majeshi; hata haitawaachia shina wala tawi.” Uharibifu wa mfumo huu mwovu wa mambo utakuwa kamili kadiri gani? Utakuwa kama mti ambao mizizi yake imeharibiwa kabisa ili usipate kukua tena.

      2. Maandiko fulani yanafafanuaje ile siku ya Yehova?

      2 Huenda ukauliza, ‘Ni “siku” gani hiyo inayotabiriwa na nabii Malaki?’ Ni siku ileile inayotajwa katika andiko la Isaya 13:9, linalosema: “Tazama, siku ya BWANA inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.” Andiko la Sefania 1:15 linatoa ufafanuzi huu linaposema: “Siku ile ni siku ya ghadhabu, siku ya fadhaa na dhiki, siku ya uharibifu na ukiwa, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza kuu.”

      “Dhiki Kubwa”

      3. ‘Siku ya Yehova’ ni nini?

      3 Katika utimizo mkubwa wa unabii wa Malaki, ‘siku ya Yehova’ ni wakati wa “dhiki kubwa.” Yesu alitabiri hivi: “Maana ndipo kutakuwa na dhiki kubwa ya namna ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu hadi sasa, la, wala haitatukia tena.” (Mathayo 24:21) Ebu fikiria jinsi ulimwengu ulivyopata dhiki, hasa tangu mwaka wa 1914. (Mathayo 24:7-12) Watu zaidi ya milioni 50 walikufa katika Vita ya Pili ya Ulimwengu! Hata hivyo, “dhiki kubwa” itafanya matukio hayo kuwa duni. Dhiki kubwa sawa na siku ya Yehova itaisha wakati wa Har–Magedoni, na kukomesha siku za mwisho za mfumo huu mwovu.—2 Timotheo 3:1-5, 13; Ufunuo 7:14; 16:14, 16.

      4. Ni nini kitakachotokea mwishoni mwa siku ya Yehova?

      4 Mwishoni mwa siku hiyo ya Yehova, ulimwengu wa Shetani na wale wanaouunga mkono watakuwa wameangamizwa. Dini isiyo ya kweli ndiyo itakayoharibiwa kwanza. Kisha Yehova atatekeleza hukumu yake dhidi ya mfumo wa Shetani wa kisiasa na wa kiuchumi. (Ufunuo 17:12-14; 19:17, 18) Ezekieli atabiri hivi: “Watatupa fedha yao katika njia kuu za mji, na dhahabu yao itakuwa kama kitu cha unajisi; fedha yao na dhahabu yao hazitaweza kuwaokoa siku ya ghadhabu ya BWANA.” (Ezekieli 7:19) Andiko la Sefania 1:14 lasema hivi kuhusu siku hiyo: “Hiyo siku ya BWANA iliyo kuu i karibu; i karibu, nayo inafanya haraka sana.” Kwa kuzingatia yale ambayo Biblia inasema kuhusu siku ya Yehova, twapaswa kuazimia kutenda kupatana na matakwa ya Mungu ya uadilifu.

  • Ni Nani Atakayeokoka Siku ya Yehova?
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Mei 1
    • 9. Unabii wa Malaki ulitimizwaje kwa mara ya kwanza?

      9 Maneno hayo yalitimia pia katika karne ya kwanza W.K. Mabaki wa Wayahudi walimtumikia Yehova na wakawa sehemu ya “taifa” jipya la Wakristo waliotiwa mafuta kwa roho. Baadaye taifa hilo lilitia ndani watu wasio Wayahudi. Lakini Waisraeli wengi wa asili walimkataa Yesu. Kwa hiyo, Yesu aliliambia hivi taifa hilo la Israeli “Tazameni! Nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.” (Mathayo 23:38; 1 Wakorintho 16:22) Katika mwaka wa 70 W.K., kama ilivyotabiriwa kwenye Malaki 4:1, ‘siku inayowaka kama tanuru’ iliwajilia Waisraeli wa asili. Yerusalemu na hekalu lake liliharibiwa, na watu zaidi ya milioni moja wakafa kwa sababu ya njaa, kung’ang’ania mamlaka, na mashambulizi yaliyofanywa na majeshi ya Roma. Hata hivyo, wale waliomtumikia Yehova hawakupatwa na dhiki hiyo.—Marko 13:14-20.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki