-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1994 | Agosti 15
-
-
Mzizi unapopatwa na madhara, baki la mti huathiriwa pia. (Linganisha Mathayo 3:10; 13:6.) Kulingana na hilo, Malaki aliandika hivi: “Siku ile inayokuja itawateketeza, asema BWANA wa majeshi; hata haitawaachia shina [“mzizi,” NW] wala tawi.” (Malaki 4:1) Maana ni wazi—kukatiliwa mbali kabisa. Wazazi (mizizi) wangekatiliwa mbali, pamoja na wazao wao (vitawi).a Hilo lakazia daraka walio nalo wazazi kuelekea watoto wao wadogo; wakati ujao udumuo wa watoto wadogo ungeweza kuamuliwa kwa msimamo wa wazazi wao mbele ya Mungu.—1 Wakorintho 7:14.
Lugha iliyo kwenye Isaya 37:31 na Malaki 4:1 yatokana na jambo la kwamba vitawi (na matunda yaliyo juu ya matawi ya chini) hupata uhai wavyo kutoka kwa mzizi. Huo ndio ufunguo wa kuelewa jinsi Yesu ni “mzizi wa Yese” na “mzizi wa Daudi.” (NW)
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1994 | Agosti 15
-
-
a Mchoro wa kaburini wa Foinike ya kale ulitumia lugha inayofanana na hiyo. Ulisema hivi juu ya wowote waliofungua kaburi hilo: “Na wasiwe wala na mzizi chini wala na matunda juu!”—Vetus Testamentum, Aprili 1961.
-