-
Kitabu Cha Biblia Namba 39—Malaki“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
4. Ni nini kinachothibitisha kitabu cha Malaki ni asilia na chenye pumzi ya Mungu?
4 Kitabu cha Malaki kimekubaliwa sikuzote na Wayahudi kuwa asilia. Manukuu yaliyo katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo kutokana nacho, hesabu fulani kati yayo ikiwa yaonyesha utimizo mbalimbali wa unabii wacho, yathibitisha kwamba kitabu cha Malaki kilipuliziwa na Mungu na ni sehemu ya vitabu vinavyokubalika vya Maandiko ya Kiebrania yaliyotambuliwa na kundi la Kikristo.—Mal. 1:2, 3—Rum. 9:13; Mal. 3:1—Mt. 11:10 na Luka 1:76 na 7:27; Mal. 4:5, 6—Mt. 11:14 na 17:10-13, Mk. 9:11-13 na Luka 1:17.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 39—Malaki“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
15. “Eliya” wa unabii wa Malaki ni nani?
15 Kisha, katika Malaki 4:5, 6, Yehova aliahidi hivi: “Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii.” “Eliya” huyu ni nani? Yesu na pia malaika aliyetokea Zekaria watumia maneno hayo kuhusu Yohana Mbatizaji, kuonyesha kwamba yeye ndiye “atatengeneza yote” na “kuwekea Bwana [Yehova, NW] tayari watu waliotengenezwa” ili wampokee Mesiya. Hata hivyo, pia Malaki asema kwamba “Eliya” ni mtangulizi wa “siku ile ya BWANA [Yehova, NW], iliyo kuu na kuogofya,” hivyo kudokeza utimizo wa wakati ujao katika siku ya hukumu.—Mt. 17:11; Luka 1:17; Mt. 11:14; Mk. 9:12.
-