-
Kitabu Cha Biblia Namba 39—Malaki“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
12. Ni nini kinachoahidiwa juu ya siku ya Yehova yenye kutia hofu?
12 Siku ya Yehova iliyo kuu na yenye kutia hofu (4:1-6). Hiyo ndiyo siku inayokuja ambayo itameza waovu, isiache wala mzizi wala tawi. Lakini jua la uadilifu litaangazia wale wanaohofu jina la Yehova, nao wataponywa. Yehova awaonya kwa upole wakumbuke Sheria ya Musa. Yehova aahidi kutuma nabii Eliya kabla ya siku yake kuu yenye kutia hofu. “Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana [kwa kuitoa kwenye uharibifu, NW].”—4:6.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 39—Malaki“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
15. “Eliya” wa unabii wa Malaki ni nani?
15 Kisha, katika Malaki 4:5, 6, Yehova aliahidi hivi: “Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii.” “Eliya” huyu ni nani? Yesu na pia malaika aliyetokea Zekaria watumia maneno hayo kuhusu Yohana Mbatizaji, kuonyesha kwamba yeye ndiye “atatengeneza yote” na “kuwekea Bwana [Yehova, NW] tayari watu waliotengenezwa” ili wampokee Mesiya. Hata hivyo, pia Malaki asema kwamba “Eliya” ni mtangulizi wa “siku ile ya BWANA [Yehova, NW], iliyo kuu na kuogofya,” hivyo kudokeza utimizo wa wakati ujao katika siku ya hukumu.—Mt. 17:11; Luka 1:17; Mt. 11:14; Mk. 9:12.
-