Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wakati wa Kujaribu na Kupepeta
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Juni 15
    • Wakati wa Kujaribu na Kupepeta

      “Na ghafula Bwana wa kweli atakuja katika hekalu lake, ambaye ninyi watu mnamtafuta, na mjumbe wa agano . . . na lazima yeye akae kama msafishaji na mtakasaji.”​—MALAKI 3:1, 3, NW.

      1, 2. (a) Ni hali zipi zilizokuwapo miongoni mwa watu wa Mungu katika karne ya tano K.W.K.? (b) Kwa sababu gani unabii wa Malaki unapaswa kutupendeza sisi?

      “MUNGU mwenye kuhukumu yuko wapi?” Wale ambao walizusha swali hilo lenye kutokeza mwito wa ushindani huko nyuma katika karne ya tano K.W.K. pia walibisha: “Kumtumikia Mungu hakuna faida.” Kuharibika kidini na kiadili miongoni mwa watu wa Mungu mwenyewe, Wayahudi, kulikuwa kumetokeza mashaka kuhusu hukumu ya kimungu. Lakini macho ya Mungu wa kweli, asiyelala usingizi, yalikuwa juu yao. Na yeye alimpa nabii Mwebrania Malaki utume wa kuwafahamisha kwamba kazi ya kusafisha, wakati wa kujaribu na kupepeta, ulikuwa mbele. Wangejua alipokuwa “Mungu mwenye kuhukumu” wakati angekuja kwa ghafula kuhukumu!​—Malaki 2:17; 3:1, 14, 15.

  • Wakati wa Kujaribu na Kupepeta
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Juni 15
    • Utimizo wa Karne ya Kwanza

      9. Katika utimizo wa unabii wa Malaki, “mjumbe” alikuwa nani? Kwa sababu gani unajibu hivyo?

      9 Akizungumza kutoka katika kiti chake cha enzi kilichoinuliwa juu sana mbinguni, Hakimu Mkuu anasema: “Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu.” (Malaki 3:la) “Mjumbe” huyo alikuwa nani? Mwandikaji wa Biblia Marko anaunganisha maunabii ya Malaki 3:1 na Isaya 40:3 na anayatumia yote mawili kuhusu Yohana Mbatizaji. (Marko 1:1-4) Yesu Kristo, pia, baadaye alimtambulisha Yohana kuwa huyo “mjumbe.” (Mathayo 11:10-14) Hivyo ilikuwa katika masika ya 29 W.K., kwamba Yohana mbatizaji alianza kazi akiwa “mjumbe,” mtangulizi. Yeye alikuwa aitayarishe njia kwa ajili ya kuja kwa Yehova katika hukumu kwa kuwatayarisha Waisraeli kwa ajili ya kuja kwa Mwakilishi Mkuu wa Mungu, Yesu Kristo.

      10. Yohana Mbatizaji alitumikaje “kumwekea Bwana [Yehova, IVW] tayari watu waliotengenezwa”? (Luka 1:17)

      10 Kupelekwa kwa Yohana kabla ya wakati kulikuwa wonyesho wa fadhili-zisizostahilika za Mungu kuwaelekea Wayahudi. Katika uhusiano wa agano pamoja na Yehova, walihitaji kutubu kwa ajili ya dhambi zao dhidi ya Sheria. Yohana alinyosha mambo ya kidini na akafunua wazi unafiki wa kidini. (Mathayo 3:1-3, 7-12) Aliamsha Wayahudi wenye mioyo minyofu kumtazamia Kristo ili waweze kumfuata Yeye.​—Yohana 1:35-37.

      11. Tunaweza kumtambuaje “Bwana [wa kweli]” ambaye angekuja kwenye hekalu kwa ghafula?

      11 Unabii wa Malaki unaendelea kusema: “Naye Bwana mnayemtafuta atalijilia hekalu lake ghafula; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja, asema Bwana [Yehova, NW], wa majeshi.” (Malaki 3:lb) Ni nani aliyekuwa “Bwana [wa kweli],” ambaye angekuja kwenye hekalu lake “ghafula,” au bila kutazamiwa? Usemi wa Kiebrania unaotumiwa ni ha·’A·dhohnʹ . Matumizi ya neno kidhihirisho ha (‘yule’) kabla ya jina la cheo, ‘A·dhohnʹ (“Bwana; Bwana-Mkubwa”) yanawekea mpaka matumizi ya jina hili la cheo kwa Yehova Mungu peke yake. Kwa kweli, lilikuwa “hekalu lake” ambamo Yehova angekuja.​—Habakuki 2:20; Zaburi 11:4.

      12. “Yule mjumbe wa agano” ni nani, naye ni “yule mjumbe” wa “agano” lipi?

      12 Baada ya kumtaja mjumbe mmoja, Malaki alionyesha kwamba “Bwana [wa kweli],” angekuja kwenye “hekalu lake” akiwa pamoja na mjumbe fulani tofauti, “yule mjumbe wa agano.” Huyo angekuwa nani? Basi, kwa sababu ya vile mambo yalivyotukia, ni jambo la akili kukata shauri kwamba “yule mjumbe wa agano” ni Yesu Kristo, ambaye Yohana Mbatizaji alimjulisha kwa wanafunzi wake kuwa “Mwana-Kondoo wa Mungu.” (Yohana 1:29-34) Masihi “yule mjumbe” ni wa “agano” jipi? Ushuhuda wa Luka 1:69-75 na Matendo 3:12, 19-26 unadokeza kwamba ni agano la Kiabrahamu, ambalo kwa msingi walo Wayahudi walikuwa wa kwanza kupewa nafasi ya kuwa warithi wa Ufalme.

      13. Ni kwa maana gani yule “Bwana [wa kweli]” Yehova angekuja kwenye hekalu?

      13 Yule “Bwana [wa kweli]” hakuja yeye mwenyewe kwenye hekalu halisi katika Yerusalemu. (1 Wafalme 8:27) Alikuja kwa njia ya kuwakilishwa, yaani, kupitia kwa “mjumbe wa agano,” Yesu Kristo, aliyekuja kwa jina la Yehova na kwa kuungwa mkono na roho takatifu ya Mungu.a

      14. (a) Kwa sababu gani kusafishwa kwa hekalu na Yesu katika 30 W.K. kwa wazi kulikuwa ishara tu ya jambo ambalo lingekuja kutukia? (b) Hekalu lilisafishwa katika njia gani na lini kwa utimizo wa Malaki 3:1?

      14 Katika masika ya 30 W.K., Yesu alikuja kwenye hekalu la Yehova katika Yerusalemu na akawafukuza wale ambao walikuwa wakilifanya “kuwa nyumba ya biashara.” (Yohana 2:13-16) Lakini jambo hilo lilikuwa tu ishara ya yale ambayo yangetukia kwa utimizo wa unabii wa Malaki. Kufuatia kisa hiki, Yohana, akiwa yule “mjumbe,” aliendelea kuwabatiza na kuwaelekeza wanafunzi wake kwa Yesu. (Yohana 3:23-30) Hata hivyo, katika Nisani 9, 33 W.K., Yesu aliingia kwa shangwe katika Yerusalemu, akijitokeza mwenyewe kuwa Mfalme. (Mathayo 21:1-9; Zekaria 9:9) Yohana alikuwa ameimaliza kazi yake, akiwa amekatwa kichwa na Herode karibu mwaka mmoja mbele. Hivyo wakati Yesu alipokuja kwenye hekalu katika Nisani 10, alikuja kwa njia rasmi akiwa “yule mjumbe wa agano,” akiwa mwakilishi wa kuhukumu wa yule “Bwana [wa kweli]” Yehova, kwa utimizo wa Malaki 3:1. Yesu alilisafisha hekalu, akiwafukuza wale ambao walikuwa wakifanya biashara humo, akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadili fedha. Yeye alizidi kusema: “Je! haikuandikwa [katika Isaya 56:7], Nyumba ya [Yehova] itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote? Bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.”​—Marko 11:15-18.

      15. Kama jamii, viongozi wa kidini wa Kiyahudi waliitikiaje kazi ya kusafisha, lakini ni jambo gani lililokuwa kweli kuhusu makuhani fulani?

      15 Hivyo taarifa ilitolewa kwa viongozi wa kidini wa Israeli kwamba wakati wao ulikuwa umefika. Kama jamii, walikataa kumkubali “mjumbe wa agano” wa Yehova. Wao ‘hawakuistahimili siku ya kuja kwake’ kwa kuwa wao walikataa kutii kwa unyenyekevu kazi ya kusafisha ya Msafishaji Mkuu. (Malaki 3:2, 3) Walistahili kupepetwa kama wanaostahili uharibifu. Ingawaje, kwa wazi, kulikuwako na “wana wa Lawi” wengine wenye mioyo mizuri, kwa kuwa muda mfupi baada ya kifo cha Yesu “jamii kubwa ya makuhani [Walawi] wakaitii ile Imani.”​—Matendo 6:7.

  • Wakati wa Kujaribu na Kupepeta
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Juni 15
    • Utimizo wa Ki-siku-hizi

      17. Ni jambo gani linaloonyesha kwamba unabii wa Malaki ungepata utimizo zaidi katika nyakati za kisasa?

      17 Lakini namna gani utimizo wa pili, au wa ki-siku-hizi wa unabii wa Malaki? Katika karne ya kwanza, utimizo wa kwanza ulifuata kupakwa mafuta kwa Yesu kwa roho takatifu ili awe Mfalme-Mchaguliwa wa Ufalme wa Mungu. Kulingana na kufikiri kuzuri, kwapaswa kuwe na utimizo zaidi ya unabii huo baada ya Yesu Kristo kutawazwa katika mbingu katika 1914. Unabii wenyewe unaonyesha kwamba ungetimizwa “kabla haijaja siku ile ya Bwana [Yehova, NW].” (Malaki 4:5) Ingawa “siku ya Bwana [Yehova, NW]” iliufikia mfumo wa Kiyahudi katika 70 W.K., Maandiko yanaelekeza mbele kwenye “siku ya Bwana [Yehova, NW]” iliyo mbele wakati huu wa “kuwapo” kwa Kristo.​—Mathayo 24:3, NW; 2 Wathesalonike 2:1, 2; 2 Petro 3:10-13.

      18. Katika 1922, watu wa Mungu walifahamishwaje kwamba walikuwa katika wakati wa hukumu?

      18 Mapema kama 1922, watu wa Yehova walikuwa wamejulishwa kwamba walikuwa katika wakati wa hukumu kwa utimizo wa unabii wa Malaki. Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) wa Septemba 1 ulisema: “Lakini unabii wa Malaki unatazama mbele kupita utimizo wa sehemu tu wakati wa kuja kwa mara ya kwanza kwa Bwana wetu, na kuelekeza mbele kwenye wakati ambao Masihi apaswa aje katika utukufu na uwezo, na wakati ambao apaswa ahukumu miongoni mwa watu wake . . . Sasa, kwa mara nyingine, wakati wa hukumu umefika; tena watu wanaojidai kuwa wake wanajaribiwa kama kwamba kwa moto, na wana wa Lawi wenye mioyo ya kweli wanakusanywa pamoja kwa utumishi.”

      19. Katika utimizo wa kisasa, ni kwa njia ipi “mjumbe” alipelekwa kabla ya wakati?

      19 Kama inavyoonyeshwa kwenye Malaki 3:1, mjumbe wa pekee alitumwa kabla ya wakati. Huyo alithibitika kuwa, si mtu mmoja, bali jamii inayotumikia kama Yohana Mbatizaji. Tangu 1881 jamii hii imetumia kinachojulikana sasa kuwa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti katika kazi yenye kutokeza ya kuelimisha watu Biblia. Jambo hili limetokeza kurudishwa kwa kweli nyingi za msingi kwa mioyo ya wanaopenda Biblia. Mengine ya mambo hayo yaliyoelezwa wazi ni: Mwanadamu hana nafsi isiyoweza kufa, bali yeye ni nafsi; hakuna moto wenye mateso; Yesu Kristo hangerudi katika mwili; Yehova ni Mungu mmoja, si utatu. Kwa kweli, ilikuwa kazi ambayo ‘ilitengeneza njia mbele ya [Yehova]’ kwa kazi yake ya kuhukumu.

      20. (a) Kwa wazi, ni lini Yehova alipokuja kwenye hekalu? (b) Jambo hili linatokeza maswali gani?

      20 Kwa ghafula, Yehova, akiwa “Bwana [wa kweli],” alikuja kwenye hekalu lake la kiroho. Wakati gani? Kiolezo kiliwekwa katika utimizo wa karne ya kwanza. Huko nyuma Yesu alikuja na akalisafisha hekalu miaka mitatu na nusu baada ya kupakwa-mafuta akiwa Mfalme katika Mto Yordani. Kwa kushikamana na kiolezo hicho, tangu Yesu alipotawazwa kuwa Mfalme katika wakati wa vuli wa 1914, linaonekana kuwa jambo la akili kwamba miaka mitatu na nusu baadaye yeye angetazamiwa aambatane na “Bwana [wa kweli] Yehova kwenye hekalu la kiroho. Kulingana na unabii huo, ni jambo gani ambalo lingetukia kuanzia wakati huo na kuendelea? Kujaribiwa na kupepetwa. Lakini jambo hili linatokeza maswali ya maana sana: Kuna ushuhuda gani wa kusafisha huku? Je! kunaendelea mpaka wakati huu wa kisasa? Na hayo yote yanakuhusuje wewe binafsi? Ebu na tuone.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki