Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu Cha Biblia Namba 39—Malaki
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 4. Ni nini kinachothibitisha kitabu cha Malaki ni asilia na chenye pumzi ya Mungu?

      4 Kitabu cha Malaki kimekubaliwa sikuzote na Wayahudi kuwa asilia. Manukuu yaliyo katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo kutokana nacho, hesabu fulani kati yayo ikiwa yaonyesha utimizo mbalimbali wa unabii wacho, yathibitisha kwamba kitabu cha Malaki kilipuliziwa na Mungu na ni sehemu ya vitabu vinavyokubalika vya Maandiko ya Kiebrania yaliyotambuliwa na kundi la Kikristo.—Mal. 1:2, 3—Rum. 9:13; Mal. 3:1—Mt. 11:10 na Luka 1:76 na 7:27; Mal. 4:5, 6—Mt. 11:14 na 17:10-13, Mk. 9:11-13 na Luka 1:17.

  • Kitabu Cha Biblia Namba 39—Malaki
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 10. Ni kwa ajili ya kazi gani ya hukumu Bwana aja kwenye hekalu lake?

      10 Bwana wa kweli na mjumbe (3:1-18). Sasa unabii huu wafikia upeo kwa maneno ya “BWANA [Yehova, NW] wa majeshi”: “Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu; naye Bwana mnayemtafuta atalijilia hekalu lake ghafula; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja.” (3:1) Akiwa mtakatishaji, Yeye atasafisha wana wa Lawi na atakuwa shahidi wa kasi juu ya waovu ambao wamekuwa hawamwogopi Yeye. Yehova habadiliki, na kwa sababu wao ni wana wa Yakobo, yeye atawarudia kwa rehema ikiwa wao watamrudia yeye.

  • Kitabu Cha Biblia Namba 39—Malaki
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 14. (a) Malaki aelekeza mbele kwenye nini, hasa? (b) Malaki 3:1 ulitimizwaje katika karne ya kwanza W.K.?

      14 Kikiwa ndicho kitabu cha mwisho cha Maandiko ya Kiebrania yaliyopuliziwa na Mungu, Malaki chaelekeza mbele kwenye matukio yanayozunguka kuja kwa Mesiya, ambaye kutokea kwake zaidi ya karne nne baadaye kulitoa sababu ya kuandikwa kwa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kama ilivyoandikwa katika Malaki 3:1, Yehova wa majeshi alisema: “Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu.” Akinena akiwa na pumzi ya Mungu, Zekaria mwenye umri mkubwa alionyesha kwamba hilo lilitimizwa katika mwanae, Yohana Mbatizaji. (Luka 1:76) Yesu Kristo alithibitisha hilo, akieleza hivi wakati uo huo: “Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.” Yohana alikuwa ametumwa, kama alivyotabiri Malaki, ‘atengeneze njia,’ hivi kwamba yeye hakuwa miongoni mwa wale ambao Yesu alifanya nao baadaye agano kwa ajili ya Ufalme.—Mt. 11:7-12; Luka 7:27, 28; 22:28-30.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki