Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Habari Njema Lazima Zihubiriwe Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Januari 1
    • 15. (a) Ni maagizo gani ambayo Yesu aliwapa wanafunzi wake wakati yeye alipowatuma nje kuhubiri? (b) Ni jinsi gani waelezaji fulani wa Biblia wameeleza jambo hilo?

      15 Wakati Yesu alipotuma wanafunzi wake waende nje kuhubiri, yeye aliwatuma waendee watu moja kwa moja pia. Jambo hilo linaonwa katika maagizo yake yaliyoandikwa kwenye Mathayo 10:1-15, 40-42. Katika mstari 11, NW, yeye alisema: “Ndani ya mji wo wote ambamo ninyi mnaingia, tafuteni-tafuteni ni nani humo anayestahili, na kukaa humo mpaka ninyi mwondoke.” The Jerusalem Bible inafasiri mstari huu hivi: “Ombeni mpewe mtu fulani anayeitibariwa,” kama kwamba wanafunzi walipaswa kuomba mtu fulani mashuhuri au mwenye maarifa katika kijiji kile aangalie-angalie ni nani mwenye sifa njema ambaye kwa sababu hiyo alistahili ule ujumbe. (Ona pia Weymouth na King James Version.) Na hilo ndilo elezo ambalo waelezaji fulani wa Biblia wanatoa juu ya mstari 11.

  • “Habari Njema Lazima Zihubiriwe Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Januari 1
    • 17. Ni jambo gani ambalo linathibitisha kwamba wanafunzi wa Yesu hawakuwa wakitembelea watu wenye kustahili kwa kutegemea msingi wa kupendekezewa kwamba wafanye hivyo au kwa kuagana na watu kwamba wawatembelee?

      17 Jambo hilo linaonwa katika maneno ya Yesu kwenye Mathayo 10:14 “Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu.” Yesu alikuwa akisema juu ya kufanya kwa wanafunzi wake ziara za kuendea watu bila kualikwa ili kuwahubiria. Ni kweli, wao wangekubali pia kulala nyumbani mwa moja ya nyumba zile ambazo ziliitikia ule ujumbe. (Mathayo 10:11) Lakini jambo kubwa lilikuwa ile kazi ya kuhubiri. Kwenye Luka 9:6 (NW) Inasemwa hivi: “Ndipo wakianza kuondoka wakaenda wakipitia lile eneo kutoka kijiji kwa kijiji wakitangaza zile habari njema na kufanya maponyo kila mahali.” (Ona pia Luka 10:8, 9.) Wenye kustahili ambao waliwapokea wanafunzi hao ndani ya makao yao kama manabii, labda wakiwapa “kikombe cha maji baridi” au hata mahali-mahali pa kulala, hawangepoteza thawabu yao. Wao wangesikia ule ujumbe wa Ufalme.—Mathayo 10:40-42.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki