-
Tayari Kuhubiri Licha ya MatesoYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Kwa sababu kazi ya kuhubiri ni muhimu sana, Yesu anawahimiza wafuasi wake wawe na busara, ili waendelee kufanya kazi hiyo kwa uhuru. Anasema: “Mnapoteswa katika jiji moja, kimbilieni jiji lingine; kwa kweli ninawaambia, hamtamaliza kamwe kuzunguka majiji ya Israeli kabla ya Mwana wa binadamu kufika.”—Mathayo 10:23.
-
-
Tayari Kuhubiri Licha ya MatesoYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Ni wazi kwamba Yesu anafikiria wakati ujao anapowaambia mitume mambo hayo. Fikiria maneno aliyosema, kwamba wanafunzi wake hawatamaliza “kuzunguka majiji ya Israeli kabla ya Mwana wa binadamu kufika.” Yesu anaonyesha kuwa mitume wake hawatamaliza kuhubiri kuhusu Ufalme wa Mungu kabla ya Mfalme aliyetukuzwa, Yesu Kristo kufika akiwa hakimu wa Mungu.
-