-
Nani Atakuwa Mwenye Kukubaliwa na Yehova?Mnara wa Mlinzi—1988 | Novemba 15
-
-
2 Baada ya Yohana kukubaliana naye kwa moyo wa kiasi halafu Yesu akaja juu kutoka majini, “mbingu zilifunuka, na akaona roho ya Mungu ikishuka kama njiwa.” Zaidi ya hilo, “kulikuwako sauti kutoka katika mbingu iliyosema: ‘Huyu ndiye Mwanangu, mpendwa, ambaye mimi nimekubali.’ “(Mathayo 3:16, 17; Marko 1:11, NW) Lo, tamko rasmi lililoje! Sisi sote huona shangwe kufurahisha mtu fulani tunayestahi. (Matendo 6:3-6; 16:1, 2; Wafilipi 2:19-22; Mathayo 25:21) Basi, wazia jinsi wewe ungehisi ikiwa Mungu mwenye nguvu zote angetangaza, ‘Mimi nimekukubali wewe!’
-
-
Nani Atakuwa Mwenye Kukubaliwa na Yehova?Mnara wa Mlinzi—1988 | Novemba 15
-
-
Maneno Yake Yalimaanisha Nini?
4. (a) Ni nini maana ya neno la Kigiriki la ‘mwenye kukubaliwa’ katika tangazo la Mungu? (b) Kwa nini utumizi walo katika kisa hiki una upendezi wa pekee?
4 Kumbukumbu za maandishi ya Gospeli juu ya maneno ya Mungu “Nimekubali [Yesu]” zinatumia kitenzi cha Kigiriki eu·do·keʹo. (Mathayo 3:17; Marko 1:11; Luka 3:22) Kinamaanisha “kuwa mwenye kufurahika sana, kuchukua kitu kwa njia yenye kupendeleka, kupata upendezo katika,” na namna yake ya nomino ina maana ya “nia njema, ufurahio mwema, upendeleo, utakio, tamaa.” Eu·do·keʹo haihusu kibali cha kimungu tu. Mathalani, Wakristo katika Makedonia ‘walipendezwa’ kushirikiana kifedha pamoja na wengine. (Warumi 10:1; 15:26; 2 Wakorintho 5:8; 1 Wathesalonike 2:8; 3:1) Na bado, kibali ambacho Yesu alipokea kilionyeshwa na Mungu, si na wanadamu. Mtajo huo umetumiwa kwa kurejezea Yesu peke yake baada ya yeye kubatizwa. (Mathayo 17:5; 2 Petro 1:17) Kwa kupendeza, Luka 2:52, NW, inatumia neno tofauti—khaʹris—katika kunena juu ya Yesu akiwa kijana asiyebatizwa ambaye alipokea “upendeleo” kutoka kwa Mungu na wanadamu.
-