Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Yehova Mungu Wako Ndiye Unayepaswa Kumwabudu”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 1, 2. Kwa nini Yesu alienda katika nyika ya Yudea majira ya vuli ya mwaka wa 29 W.K., na nini kilichompata huko? (Tazama picha kwenye ukurasa huu.)

      NI MWANZO wa majira ya vuli ya mwaka wa 29 W.K., na Yesu yuko katika nyika ya Yudea kaskazini ya Bahari ya Chumvi. Baada ya kubatizwa na kutiwa mafuta, aliongozwa na roho takatifu kwenda kwenye eneo hilo. Akiwa huko, katikati ya eneo lenye ukame, miamba na mabonde, Yesu ametumia siku 40 akifunga, kusali, na kutafakari akiwa peke yake. Labda wakati huo, Yehova amewasiliana na Mwana wake na kumtayarisha kwa ajili ya kazi iliyo mbele yake.

      2 Sasa, Yesu akiwa amedhoofika kwa sababu ya njaa, Shetani anamwendea. Jambo linalotokea linafunua suala muhimu sana ambalo linawahusu watu wote wanaoipenda ibada safi, kutia ndani wewe.

  • “Yehova Mungu Wako Ndiye Unayepaswa Kumwabudu”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 3, 4. (a) Shetani alianza majaribu mawili ya kwanza kwa maneno gani, na huenda alikuwa akijaribu kumfanya Yesu awe na shaka kuhusu nini? (b) Shetani anatumiaje mbinu kama hizo leo?

      3 Soma Mathayo 4:1-7. Shetani anaanza majaribu yake ya kwanza mawili kwa maneno haya ya ujanja, “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu.” Je, Shetani alikuwa na shaka kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu? Hapana. Malaika huyo mwasi aliyekuwa mwana wa Mungu alijua vizuri kwamba Yesu ni Mwana mzaliwa wa kwanza wa Mungu. (Kol. 1:15) Bila shaka, Shetani pia aliyajua maneno haya ambayo Yehova alisema kutoka mbinguni wakati wa ubatizo wa Yesu: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa, ambaye nimemkubali.” (Mt. 3:17) Labda Shetani alitaka Yesu afikiri kwamba Baba yake hakuwa mwaminifu na kwamba hakumjali. Katika jaribu la kwanza​—alilotaka abadili mawe yawe mikate—​ni kama Shetani aliuliza hivi: ‘Kwa kuwa wewe ni Mwana wa Mungu, kwa nini Baba yako hakupi chakula hapa nyikani?’ Katika jaribu la pili​—alilotaka aruke kutoka kwenye mnara wa hekalu—​tunaweza kusema Shetani aliuliza hivi: ‘Kwa kuwa wewe ni Mwana wa Mungu, je, unaamini kabisa kwamba Baba yako atakulinda?’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki