-
“Nitawapa Moyo Wenye Umoja”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
11 Katika kipindi chote cha giza la utawala wa dini zinazodai kuwa za Kikristo, kulikuwa na baadhi ya Wakristo wa kweli, “ngano” ambayo Yesu alitaja kwenye mfano wake. Kama Wayahudi waliokuwa uhamishoni wanaotajwa katika Ezekieli 6:9, walimkumbuka Mungu wa kweli. Baadhi yao walipinga kwa ujasiri mafundisho ya uwongo ya dini zinazodai kuwa za Kikristo. Walidhihakiwa na kuteswa. Je, Yehova alikusudia kuwaacha watu wake katika giza hilo la kiroho milele? Hapana! Kama ilivyokuwa kwa Waisraeli wa zamani, Yehova alionyesha hasira kwa kiwango kinachofaa na kwa kipindi kinachofaa cha wakati. (Yer. 46:28) Isitoshe, Yehova hakuwaacha watu wake bila tumaini. Acheni tuzungumzie tena wale Wayahudi waliokuwa uhamishoni katika Babiloni la kale na tuone jinsi Yehova alivyowapa tumaini la kuwatoa utekwani.
Kwa karne nyingi, Wakristo wa kweli walikabili mateso mikononi mwa Babiloni Mkubwa (Tazama fungu la 10, 11)
-