Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Yehova Mungu Wako Ndiye Unayepaswa Kumwabudu”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 3, 4. (a) Shetani alianza majaribu mawili ya kwanza kwa maneno gani, na huenda alikuwa akijaribu kumfanya Yesu awe na shaka kuhusu nini? (b) Shetani anatumiaje mbinu kama hizo leo?

      3 Soma Mathayo 4:1-7. Shetani anaanza majaribu yake ya kwanza mawili kwa maneno haya ya ujanja, “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu.” Je, Shetani alikuwa na shaka kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu? Hapana. Malaika huyo mwasi aliyekuwa mwana wa Mungu alijua vizuri kwamba Yesu ni Mwana mzaliwa wa kwanza wa Mungu. (Kol. 1:15) Bila shaka, Shetani pia aliyajua maneno haya ambayo Yehova alisema kutoka mbinguni wakati wa ubatizo wa Yesu: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa, ambaye nimemkubali.” (Mt. 3:17) Labda Shetani alitaka Yesu afikiri kwamba Baba yake hakuwa mwaminifu na kwamba hakumjali. Katika jaribu la kwanza​—alilotaka abadili mawe yawe mikate—​ni kama Shetani aliuliza hivi: ‘Kwa kuwa wewe ni Mwana wa Mungu, kwa nini Baba yako hakupi chakula hapa nyikani?’ Katika jaribu la pili​—alilotaka aruke kutoka kwenye mnara wa hekalu—​tunaweza kusema Shetani aliuliza hivi: ‘Kwa kuwa wewe ni Mwana wa Mungu, je, unaamini kabisa kwamba Baba yako atakulinda?’

  • “Yehova Mungu Wako Ndiye Unayepaswa Kumwabudu”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 5. Yesu alijibuje majaribu mawili ya kwanza?

      5 Fikiria jinsi Yesu alivyojibu majaribu hayo mawili ya kwanza. Hakushuku kamwe kwamba Baba yake anampenda, naye alimtumaini kabisa Baba yake. Bila kusita, Yesu alimpinga Shetani kwa kunukuu Neno la Baba yake lililoongozwa na roho. Kwa kufaa, Yesu alinukuu maandiko yaliyo na jina la Mungu, Yehova. (Kum. 6:16; 8:3) Mwana wa Mungu alitumia njia bora sana kuonyesha kwamba alimtumaini Baba yake, alitumia jina Lake​—jina pekee ambalo linatoa uhakikisho kwamba Yehova atatimiza ahadi zake zote.a

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki