-
Mifano Kuhusu UfalmeYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Kisha Yesu anawaambia wanafunzi wake mifano mitatu zaidi. Kwanza, anasema: “Ufalme wa mbinguni ni kama hazina iliyofichwa katika shamba, ambayo mtu fulani aliipata na kuificha; na kwa sababu ya shangwe aliyo nayo, anaenda na kuuza kila kitu alicho nacho na kununua shamba hilo.”—Mathayo 13:44.
-
-
Mifano Kuhusu UfalmeYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Kwa kutumia mifano yote miwili, Yesu anakazia utayari wa mtu kujidhabihu kwa ajili ya mambo yenye thamani zaidi. Mfanyabiashara anauza haraka “vitu vyote alivyokuwa navyo” ili kupata lulu moja yenye thamani kubwa. Wanafunzi wa Yesu wanaweza kuelewa mfano huo kuhusu lulu yenye thamani. Na mtu anayepata hazina iliyofichwa shambani anauza “kila kitu” ili kuipata. Katika visa vyote, kuna kitu fulani chenye thamani, ambacho kinapaswa kumilikiwa na kuthaminiwa sana. Jambo hilo linaweza kulinganishwa na jinsi ambavyo mtu anajidhabihu ili kutosheleza uhitaji wake wa kiroho. (Mathayo 5:3) Baadhi ya wale wanaomsikiliza Yesu akitoa mifano hiyo wameonyesha utayari wa kufanya jitihada za kutosheleza uhitaji wao wa kiroho na kuwa wafuasi wake wa kweli.—Mathayo 4:19, 20; 19:27.
-