-
Wabarikiwa kwa Mafundisho ZaidiMnara wa Mlinzi—1987 | Aprili 15
-
-
Kisha Yesu anawabariki wanafunzi wake wenye kutaka kujua kwa mifano mitatu zaidi. Kwanza, yeye asema: “UfaIme wa mbingu ni kama hazina iliyofichwa katika shamba, ambayo mtu mmoja aliipata na kuificha; na kwa ajili ya furaha aliyo nayo anaenda zake na kuuza vitu alivyo navyo na kununua shamba hilo.”
-
-
Wabarikiwa kwa Mafundisho ZaidiMnara wa Mlinzi—1987 | Aprili 15
-
-
Yesu mwenyewe ni kama huyo mtu anayegundua hazina iliyofichwa na kama mfanya biashara huyo anayepata lulu ya thamani ya juu. Ilikuwa kama aliuza kila kitu, akaacha cheo chenye heshima katika mbingu awe mwanadamu wa chini. Kisha, akiwa mwanadamu duniani, anapatwa na mashutumu na mateso yenye chuki, alijithibitisha anafaa kuwa Mtawala wa Ufalme wa Mungu.
Mwito wenye ushindani unawekwa mbele ya wafuasi wa Yesu pia wauze kila kitu ili wapate thawabu nzuri ajabu ya kuwa ama mtawala mwenzi na Kristo au raia wa kidunia wa Ufalme. Je! sisi tutaona kuwa na ushirika katika Ufalme wa Mungu kuwa jambo fulani lenye thamani kubwa zaidi ya kila kitu kinginecho maishani, kuwa kama hazina ya bei kubwa au lulu yenye thamani kubwa?
-