-
Juya (Wavu) na Samaki Zinamaanisha Nini Kwako?Mnara wa Mlinzi—1992 | Juni 15
-
-
3. Kuelewa mifano ya Yesu kwaweza kutufaidije?
3 Kisha Yesu akatumia Isaya 6:9, 10, lililoeleza juu ya watu waliokuwa viziwi na vipofu kiroho. Hata hivyo, sisi hatuhitaji kuwa hivyo. Tukielewa na kutenda kupatana na mifano yake, twaweza kuwa wenye furaha sana—sasa na kwa wakati ujao usio na kikomo. Yesu anatutolea uhakikisho huu mchangamfu: “Heri [ni yenye furaha, NW] macho yenu, kwa kuwa yanaona; na masikio yenu, kwa kuwa yanasikia.” (Mathayo 13:16) Uhakikisho huo wahusu mifano yote ya Yesu, lakini acheni tukaze fikira zetu juu ya mfano mmoja mfupi wa juya, ulioandikwa kwenye Mathayo 13:47-50.
Mfano Wenye Maana Kubwa
4. Yesu alisimulia nini kwa njia ya mfano, kama inavyoonyeshwa kwenye Mathayo 13:47-50?
4 “Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya [wavu wa kuburutwa], lililotupwa baharini, likakusanya [samaki] wa kila namna; hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa. Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia [umalizio wa mfumo wa mambo, NW]; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki, na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.”
-
-
Juya (Wavu) na Samaki Zinamaanisha Nini Kwako?Mnara wa Mlinzi—1992 | Juni 15
-
-
7. Yesu alikuwa anaonyesha nini alipozungumza juu ya samaki?
7 Kupatana na hilo, samaki wa mfano huo husimamia wanadamu. Kwa hiyo, mstari wa 49 usemapo juu ya kutenganisha waovu na wenye haki, hurejezea, si viumbe wa baharini waadilifu au waovu, bali watu waadilifu au waovu. Vivyo hivyo, mstari wa 50 haupasi kutufanya tufikirie wanyama wa baharini wanaolia na kusaga meno yao. Hasha. Mfano huu wahusu kukusanywa kwa wanadamu na kutenganishwa kwao baadaye, jambo ambalo ni lenye uzito sana, kama matokeo yaonyeshavyo.
8. (a) Tunaweza kujifunza nini kuhusu yale yanayopata samaki wasiofaa? (b) Kwa kufikiria yale yaliyosemwa kuhusu samaki wasiofaa, sisi tunaweza kufanya mkataa gani kuhusiana na Ufalme?
8 Angalia kwamba wale samaki wasiofaa, yaani, waovu, watatupwa ndani ya tanuri ya moto, ambamo watalazimika kulia na kusaga meno yao. Mahali pengine, Yesu alihusianisha kulia na kusaga meno huko na kuwa nje ya Ufalme. (Mathayo 8:12; 13:41, 42) Na kwenye Mathayo 5:22 na 18:9, yeye hata alitaja “jehanum ya moto,” akirejezea kuangamizwa milele. Je! hilo halionyeshi jinsi lilivyo jambo la muhimu sana kupata maana ya mfano huo na kutenda kulingana nao? Sisi sote twajua kwamba hakuna wala hakutakuwa waovu katika Ufalme wa Mungu. Kwa hiyo, wakati Yesu aliposema kwamba “ufalme wa mbinguni umefanana na juya,” ni lazima awe alimaanisha kwamba kuhusiana na Ufalme wa Mungu, kuna sehemu inayofanana na juya ambayo hushushwa ikusanye aina tofauti-tofauti za samaki.
-