-
Kumtumikia Yehova kwa Roho ya KujidhabihuMnara wa Mlinzi—1993 | Juni 1
-
-
2. Itikio la Petro lilikuwa nini kwa maneno ya Yesu kuhusu kuteseka Kwake kwa wakati ujao, na Yesu aliitikiaje?
2 Ni muda mfupi ambao umebaki kabla ya Yesu kufa. Lakini Petro, akasirishwa na wazo hilo lionekanalo kuwa lenye kuhofisha sana. Hawezi kukubali kwamba kwa kweli Mesiya atauawa. Kwa hiyo, Petro athubutu kumkemea Bwana-Mkubwa wake. Akichochewa na nia njema kabisa, yeye asihi hivi bila kufikiri: “Hasha, [ujihurumie, NW] Bwana, hayo hayatakupata.” Lakini mara hiyo Yesu alikatalia mbali fadhili ya Petro isiyofaa, kwa hakika kama vile mtu angeponda kichwa cha nyoka mwenye sumu. “Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”—Mathayo 16:22, 23.
3. (a) Petro alijifanyaje mwakilishi wa Shetani bila kukusudia? (b) Petro alikuwaje kikwazo kwa mwendo wa kujidhabihu?
3 Bila kukusudia Petro amejifanya mwenyewe mwakilishi wa Shetani. Jibu kali la Yesu ni lenye kukata maneno kama vile alivyomjibu Shetani jangwani. Huko Ibilisi alijaribu kumshawishi Yesu awe na maisha ya starehe, awe na ufalme bila kuteseka. (Mathayo 4:1-10) Sasa Petro amtia moyo ajihurumie. Yesu ajua kwamba hayo si mapenzi ya Baba yake. Ni lazima maisha yake yawe ya kujidhabihu, si ya kujitosheleza. (Mathayo 20:28) Petro anakuwa kikwazo kwa mwendo huo; huruma yake yenye nia njema inakuwa mtego.a Lakini, Yesu aona kwa wazi kwamba ikiwa angekuwa na wazo lolote la maisha bila kujidhabihu, angepoteza upendeleo wa Mungu kwa kunaswa katika mtego wa kishetani wa kuleta kifo.
4. Kwa nini Yesu hakujitakia wala kuwatakia wafuasi wake maisha ya starehe ya kula raha?
4 Kwa hiyo, fikira za Petro zilihitaji kurekebishwa. Maneno yake kwa Yesu yaliwakilisha wazo la mwanadamu, si la Mungu. Maisha ya starehe ya kula raha, njia rahisi ya kuepuka kuteseka, hayakuwa ya Yesu; wala wafuasi wa Yesu hawangekuwa na maisha kama hayo, kwani Yesu aendelea kumwambia Petro na wale wanafunzi wengine hivi: “Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake [mti wake wa mateso, NW], anifuate [daima, NW].”—Mathayo 16:24.
-
-
Kumtumikia Yehova kwa Roho ya KujidhabihuMnara wa Mlinzi—1993 | Juni 1
-
-
a Katika Kigiriki, mwanzoni “kikwazo” (σκάνδαλον, skanʹda·lon) lilikuwa “jina la sehemu ya mtego ambapo chambo kinashikanishwa, kwa hiyo, mtego au tanzi yenyewe.”—Vine’s Expository Dictionary of Old and New Testament Words.
-