-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1987 | Mei 1
-
-
Ingawa hivyo, acheni tukaze fikira juu ya maana nyingine bado ambayo Biblia inatumia neno ko’smos. Inafanya hivyo kumaanisha muundo, utaratibu, au eneo lenye mipaka la maisha ya kibinadamu.a Tunakuta matumizi kama hayo katika elezo la Yesu: “Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote [ko’smos], na kupata hasara ya nafsi yake?” (Mathayo 16:26) Kwa wazi Kristo hakuwa akieleza juu ya mtu ‘kuupata ulimwengu wote wa jamii ya wanadamu’ wala ‘ulimwengu wote wa watu waliotengwa mbali na Mungu.’ Si wanadamu ambao mtu mwenye kufuatia vitu vya kimwili angeweza kuwapata, bali ni vitu ambavyo watu wanavyo, mambo wanayofanya, au wanayopanga. Ndivyo pia ilivyokuwa juu ya maoneleo ya mtume Paulo kuhusu mtu aliyefunga ndoa ‘kuhangaishwa na tamaa ya vitu vya ulimwengu.’ Vilevile, haimpasi Mkristo awe ‘akiutumia ulimwengu sana.’—1 Wakorintho 7:31-33, NW.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1987 | Mei 1
-
-
a Kamusi iliyotajwa juu inaonyesha kwamba hata katika Kigiriki cha kale, kisicho cha Kibiblia, “kosmos ndilo neno la msingi kwa utaratibu wa ulimwengu, mfumo wa ulimwengu.”
-