-
Sikiliza Sauti ya YehovaMnara wa Mlinzi (Funzo)—2019 | Machi
-
-
“MSIKILIZENI”
7. Kulingana na Mathayo 17:1-5, Yehova alizungumza kutoka mbinguni wakati wa tukio gani, naye alisema nini?
7 Soma Mathayo 17:1-5. Mara ya pili ambayo Yehova alizungumza kutoka mbinguni ni wakati Yesu ‘alipogeuka sura.’ Yesu alikuwa amemwalika Petro, Yakobo, na Yohana waende pamoja naye kwenye mlima fulani mrefu. Huko, waliona maono yenye kustaajabisha. Uso wa Yesu uling’aa na mavazi yake yalimetameta. Watu wawili, waliowakilisha Musa na Eliya, walianza kuzungumza na Yesu kuhusu kifo chake kilichokuwa kikikaribia pamoja na ufufuo wake. Ingawa mitume hao watatu walikuwa “wamelemewa na usingizi,” waliona maono hayo ya ajabu walipoamka kabisa. (Luka 9:29-32) Kisha, wingu jangavu likawafunika, nao wakasikia sauti ikitoka kwenye wingu hilo—sauti ya Mungu! Na kama ilivyokuwa wakati Yesu alipobatizwa, Yehova alionyesha kwamba Yesu ana kibali chake na anampenda, aliposema hivi: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa, ambaye nimemkubali.” Lakini pindi hii Yehova aliongeza hivi: “Msikilizeni.”
-
-
Sikiliza Sauti ya YehovaMnara wa Mlinzi (Funzo)—2019 | Machi
-
-
9. Yesu aliwapa wanafunzi wake ushauri gani unaofaa?
9 “Msikilizeni.” Yehova alitaja waziwazi kwamba anataka tumsikilize Mwanaye na tumtii. Yesu alisema nini alipokuwa duniani? Alisema mambo mengi muhimu tunayopaswa kusikiliza! Kwa mfano, upendo ulimchochea kuwafundisha wafuasi wake jinsi ya kuhubiri habari njema, na aliwakumbusha tena na tena kwamba wanapaswa kuendelea kukesha. (Mt. 24:42; 28:19, 20) Pia, aliwahimiza wajitahidi sana, na akawatia moyo wasikate tamaa. (Luka 13:24) Yesu aliwasisitizia wafuasi wake umuhimu wa kupendana, kuendelea kuwa na umoja, na kushika amri zake. (Yoh. 15:10, 12, 13) Ushauri huo wa Yesu uliwafaa kabisa wanafunzi wake! Ushauri huo ni muhimu leo pia kama tu ulivyokuwa Yesu alipoutoa.
-