-
Imani Inaweza Kuondosha Milima!Mnara wa Mlinzi—1987 | Julai 15
-
-
Yesu alieleza sababu, akisema: “Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu.“ Kisha akaendelea: “Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.“—Mathayo 17:14-20.
-
-
Imani Inaweza Kuondosha Milima!Mnara wa Mlinzi—1987 | Julai 15
-
-
Imani Inaweza Kuondosha Milima!
Hata hivyo, huenda mtu fulani akauliza, ‵Je! Yesu alimaanisha kwamba imani kama hiyo ingeweza kihalisi kuhamisha milima?ʼ Huenda Yesu akawa alitia hilo ndani, lakini mara nyingi yeye alitumia mifano. (Mathayo 13:34) Kwa hiyo pengine yeye alifikiria vizuizi ambavyo vingeweza kuwa kama milima kwa mwamini. Kwa kweli, mara nyingi neno “mlima“ linatumiwa kumaanisha kiasi kikubwa, kama vile “mlima wa madeni.“ Uhakika wa kwamba imani ya kweli inaweza kuhamisha au kuondosha vizuizi mfano wa mlima unathibitishwa na mambo mengi yaliyoonwa na watu wa kisasa.
Kwa mfano, je! wewe hungekubali kwamba mtu kuwa amepooza kutoka shingoni kwenda chini ungekuwa mlima kweli kweli? Hata hivyo, mtu aliyepooza miguu na mikono yote anayeishi katika Vancouver, B.C., Kanada, si kwamba amejifunza kupaka rangi tu, kwa kutumia brashi au kisu cha kuchanganya rangi
akikishika mdomoni mwake, bali pia anajiruzuku mwenyewe kwa kuuza michoro yake. Tena, imani yake inamsukuma awaambie wengine juu ya yale ambayo amejifunza kutoka kwa Biblia, akifanya hivyo akiwa katika kiti chake cha magurudumu au kwa kuandika barua. Yeye anachapa barua zake kwa kupiga herufi za taipureta kwa kijiti anachokishika mdomoni mwake. Pia, yeye anahudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida na kutoa hotuba katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi inayoongozwa na Mashahidi wa Yehova. Mfano wa imani yake, pamoja na kazi yake ngumu na kupiga kwake moyo konde, ni chanzo cha kitiamoyo kwa wale walio karibu naye.
-