-
Kudumisha Amani na Usafi wa KutanikoTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
14 Yesu aliorodhesha hatua hususa za kutatua matatizo yanayohusu makosa mazito yanayoweza kutokea kati ya Wakristo. Ona hatua alizotaja: “Ndugu yako akitenda dhambi, [1] nenda ufunue kosa lake kati yako na yeye peke yenu. Akikusikiliza, umempata ndugu yako. Lakini asipokusikiliza, [2] nenda pamoja na mtu mmoja au wawili, ili kwa ushahidi wa mashahidi wawili au watatu kila jambo lithibitishwe. Asipowasikiliza hao, [3] liambie kutaniko. Asipolisikiliza kutaniko pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na kama mkusanya kodi.”—Mt. 18:15-17.
-
-
Kudumisha Amani na Usafi wa KutanikoTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
18 Ikiwa umeshindwa kumpata ndugu yako kwa kuchukua hatua ya kufunua kosa lake “kati yako na yeye peke yenu,” sasa unaweza kufanya kama Yesu alivyoshauri, “nenda pamoja na mtu mmoja au wawili,” na uzungumze na ndugu yako tena. Wale unaowachukua wanapaswa pia kuwa na lengo la kumpata ndugu yako. Inafaa uchukue watu walioshuhudia kosa linalodaiwa, lakini ikiwa hakuna walioshuhudia kosa hilo, unaweza kuamua kuchukua mtu mmoja au wawili washuhudie mazungumzo hayo. Huenda wakawa na ujuzi wa jambo linalohusika na wanaweza kuamua ikiwa kwa kweli kosa lilifanywa. Ukiwachukua wazee wakashuhudie hawatawakilisha kutaniko kwa kuwa baraza la wazee halijawapa mgawo hususa wa kufanya hivyo.
-