Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Talaka Biblia Inasema Nini Hasa?
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Mei 15
    • Taarifa ya Yesu iliyonukuliwa juu ilikuwa sehemu ya jibu lake kwa swali hili la Mafarisayo: “Je! ni jambo la kisheria mwanamume kutaliki mke wake juu ya kila namna ya sababu?” (Mathayo 19:3-6, NW) Kwa kutotosheka na jibu walilopata, Mafarisayo walizidi kumswali kwa kuuliza hivi: “Mbona, basi, Musa aliamrisha kutoa cheti cha kumwondosha na kumtaliki?” Hapo basi, Yesu akasema: “Musa, kwa kufikiria ugumu wa mioyo yenu, aliwafanyia ninyi mruhusio wa kutaliki wake zenu, lakini haijawa hivyo tangu mwanzoni.” Ndipo akaongezea: “Mimi nawaambia ninyi kwamba ye yote anayetaliki mke wake, isipokuwa juu ya sababu ya uasherati, na anaoa mwingine afanya uzinzi.”​—⁠Mathayo 19:7-9, NW.

  • Talaka Biblia Inasema Nini Hasa?
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Mei 15
    • Wakati aina ya binadamu ilipopepesuka ndani ya dhambi na kutokamilika, ndoa ilipepesuka hivyo hivyo. (Warumi 5:12) Kwa kuwa wanadamu hawakuwa tena wakamilifu, mahusiano ya kibinadamu yaliingiwa na migogoro na kutiwa madoa na ubinafsi, pupa, na kujipenda. Hilo ndilo jambo ambalo Yesu alirejezea kuwa ni “ugumu wa mioyo,” jambo ambalo lilifanya Sheria ya Musa iiachie nafasi talaka. Na bado, Yesu aliwakumbusha Mafarisayo hivi: “Haijawa hivyo tangu mwanzoni.” Sasa, chini ya hali zisizokamilika, wenzi wa ndoa wanapaswa kutia jitihada inayohitajiwa kutatua magumu na matatizo yo yote badala ya kuyatumia kama sababu au maudhuru ya kuvunja ndoa yao. Hata hivyo, Yesu alionyesha kwamba kuna sababu moja ya pekee, yaani, uasherati. Ukosefu wa uaminifu katika ndoa unaweza kuwa sababu za kuvunja ndoa.

  • Talaka Biblia Inasema Nini Hasa?
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Mei 15
    • Kutokana na yaliyotangulia, ni wazi kwamba Biblia haisemi ndoa zote zinabaki zikiwa za kudumu na hakuna talaka inayoruhusiwa kwa sababu yo yote ile. Kwa upande ule mwingine, Biblia inaandaa msingi mmoja tu unaokubalika wa talaka, yaani, “sababu ya uasherati.”

      “Acheni Ndoa Iheshimike”

      Kwa kuruhusu kuwe na sababu ya talaka, je! Biblia inatia moyo talaka? Je! ruhusa hiyo inafanya ndoa iwe kitu kidogo tu au kuinyang’anya fahari yayo? Au je! kwa kuruhusu sababu moja tu ya talaka, Biblia inaweka himila ya kupita kiasi juu ya wale wanaofunga ndoa?

      Tofauti kabisa na hivyo, Biblia inasema juu ya ndoa kuwa kimoja cha vifungo vyenye ukaribu na usiri zaidi ambavyo watu wawili wanaweza kufurahia. “Mwanamume ataacha baba yake na mama yake na lazima aambatane na mke wake na wao lazima wawe mnofu mmoja,” unasema usimulizi wa Mwanzo wa ndoa ya kwanza. (Mwanzo 2:24, NW) Na wenzi wa ndoa wanapaswa kulinda uhusiano huu wa “mnofu mmoja” kuwa kitu chenye thamani kubwa. “Acheni ndoa iheshimike miongoni mwa wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi,” inashauri Biblia.​—⁠Waebrania 13:4, NW.

      Mara nyingi imesemwa, kwa njia fulani, kwamba msingi wa ndoa ya kudumu na yenye furaha si upendo wa kimahaba bali ni ukosefu wa ubinafsi. Hivyo ndivyo hasa Biblia inavyoonyesha. Inasema hivi: “Waume wanapaswa kuwa wakipenda wake zao kama miili yao wenyewe. Yeye ambaye anapenda mke wake anajipenda mwenyewe, kwa maana hakuna mtu amepata kamwe kuchukia mnofu wake mwenyewe; bali yeye anaulisha na kuutunza sana, kama vile Kristo pia anavyolifanyia kundi. . . . Kwa upande ule mwingine, mke anapaswa kuwa na staha ya kina kirefu kwa mume wake.” (Waefeso 5:28-33, NW) Na kwa usemi wa kutoboa wazi, Biblia inashauri hivi: “Acheni mume atolee mke wake haki yake; lakini acheni mke pia afanye hali kadhalika kwa mume wake. Mke hajizoezi mamlaka juu ya mwili wake mwenyewe, bali mume wake anafanya hivyo; hali kadhalika, pia, mume hajizoezi mamlaka juu ya mwili wake mwenyewe, bali mke wake anafanya hivyo. Msiwe I mkinyimana mtu na mwenzake jambo hilo “​—⁠ 1 Wakorintho 7:3-5, NW.

      Wakati wenzi wote wawili wanapokuwa na nia ya kukaa kwa kufuata mashauri hayo yenye hekima, haielekei sana kwamba ndoa yao itazorota kufikia hatua ambapo mmoja wao angegeukia mapenzi nje ya ndoa, na hivyo awe kwa kweli anaharibu ule uhusiano wa “mnofu mmoja.” Hata ikiwa mmoja wa wenzi wa ndoa hakubali kanuni hizo za Biblia, mwenzi yule mwitikadi anaweza kuwa na uhakika wa kwamba njia ya Mungu ingali ndiyo bora zaidi, na matatizo mengi ya ndoa yanaweza kutatuliwa au kuepukwa hivyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki