Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Baraka ya Yehova Inatajirisha
    Mnara wa Mlinzi—1986 | Juni 15
    • 5. Yesu alikuwa na maoni gani juu ya mali?

      5 Mara nyingi Yesu aliitaja hatari ya mali, kwa sababu inamwelekea kila mtu, wale walio na wale wasio matajiri. (Mathayo 6:24-32; Luka 6:24; 12:15-21) Ili uone msingi wa kila mtu kujichunguza binafsi, fikiria aliyoyasema Yesu katika pindi moja, kama yanavyosimuliwa katika Mathayo 19:16-24; Marko 10:17-30; na Luka 18:18-30. Kwa kweli, kwa sababu gani usitue sasa ili usome moja au yote ya masimulizi hayo?

  • Baraka ya Yehova Inatajirisha
    Mnara wa Mlinzi—1986 | Juni 15
    • 7 Baadaye Yesu alisema: “Kwa shida gani wenye mali watauingia ufalme wa Mungu! Kwa maana ni vyepesi ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.” (Luka 18:24, 25) Je! shauri hilo lilikuwa kwa mtawala huyo tajiri peke yake? Au wewe unahusika, uwe u tajiri au maskini? Acheni tuone.

      8. (a) Mtawala huyo kijana Myahudi alikuwaje? (b) Yeye alikuwa na kasoro gani, na kwa sababu gani jambo hilo lituhangaishe sisi?

      8 Unaweza kusaidiwa uifahamu hali ya mtawala huyo kijana ukiwazia hali nyingine ya kisasa inayofanana nayo​—Mkristo kijana aliye safi, mwenye maarifa mazuri ya Biblia, maadili bora, na mwenye kutoka katika jamaa yenye utajiri. Huenda ukaonea wivu mtu wa namna hiyo leo. Lakini Yesu alipata ukosefu mkubwa katika kijana yule Myahudi: Utajiri au mali zake zilikuwa za maana mno katika maisha yake. Ndiyo sababu Yesu alishauri hivyo. Unaweza kuona ni kwa nini usimulizi huo wa Biblia ni kwa ajili yetu, kama sisi ni matajiri au maskini. Pesa na mali zingeweza kuwa za maana mno kwa ye yote kati yetu, tuwe tunazo tayari au tunatamani tu kuwa nazo.

      9. Tunajuaje kwamba Yesu hakuwa akilaumu utajiri hasa?

      9 Kristo hakuwa akisema kwamba mtu mwenye mali hangeweza kumtumika Mungu. Wengi wamemtumikia. Kijana huyo Myahudi alikuwa amefanya hivyo​—kwa kadiri fulani. Alikuwako Zakayo mkusanya kodi, aliyekuwa “tajiri.” (Luka 19:2-10) Wakristo fulani wapakwa mafuta katika karne ya kwanza walikuwa matajiri na kwa hiyo walikuwa na mwito wa pekee wa ushindani kwamba “wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo.” (1 Timotheo 6:17, 18; Yakobo 1:9, 10) Na leo pia kuna Wakristo fulani matajiri. Mara nyingi wao wametoa kwa ukarimu ili kuunga mkono kazi ya Ufalme, wakaruhusu nyumba zao zitumiwe kwa ajili ya mikutano, na wakatumia magari yao katika huduma. Basi, mbona Yesu akasema vile kuhusu yule mtu tajiri na ngamia? Tunaweza kujifunza nini kutokana na maneno hayo?

      10. Tunaweza kukata neno gani kutokana na shauri la Yesu katika pindi hiyo?

      10 Kama vile wewe unavyoweza kuthamini, ni jambo moja kuanza kumwabudu Mungu; ni jambo jingine kuthibitika kuwa mwaminifu mpaka mwisho. (Mathayo 24:13; Wafilipi 3:12-14) Labda Yesu alikuwa akifikiria jambo hilo aliposema hivi: “Ni rahisi ngamia kupenya katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.” (Marko 10:25) Hakuna ngamia angeweza kujifinya apite katika jicho dogo sana la sindano ya kushonea, kwa hiyo ni wazi Yesu alikuwa akitumia msemo wa kutia chumvi usiokusudiwa kuchukuliwa kwa njia halisi. Ingawa hivyo, huo unaonyesha jinsi ilivyo vigumu kwa mtu tajiri kufanya jambo fulani. Jambo gani? Si kuanza tu kutumikia Mungu, hapana, bali “kuingia katika ufalme wa Mungu,” kupata uzima wa milele. Hata msimamo wako uwe nini kifedha, shauri la Yesu linaweza kusaidia njia yako ya kufikiri, maendeleo yako ya kiroho, na kupata uzima wenye kudumu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki