-
Mifano Miwili Kuhusu Mashamba ya MizabibuYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Hata hivyo, “wakulima” waliwatendea vibaya na kuwaua “watumwa” waliotumwa kwao. Yesu anaeleza hivi: “[Mwenye shamba la mizabibu] alikuwa na mmoja zaidi, mwana wake mpendwa. Mwishowe akamtuma kwao akisema: ‘Watamheshimu mwanangu.’ Lakini wakulima wakaambiana, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, na urithi utakuwa wetu.’ Kwa hiyo wakamkamata, wakamuua.”—Marko 12:6-8.
-
-
Mifano Miwili Kuhusu Mashamba ya MizabibuYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Waandishi na wakuu wa makuhani wanatambua kwamba “mfano aliosema uliwahusu.” (Luka 20:19) Kuliko wakati mwingine wowote, wanataka kumuua yule aliye na haki ya kuwa “mrithi.” Lakini wanauogopa umati, ambao unamwona Yesu kuwa nabii, basi hawajaribu kumuua wakati huo.
-