Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Habari Njema Inavyohubiriwa
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 4. Tunajitahidi sana ili kuwafikia watu wote

      Mashahidi wa Yehova hufanya jitihada za pekee ili kuwahubiria watu habari njema kila mahali. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

      VIDEO: Kuhubiri Katika “Sehemu ya Mbali Zaidi ya Dunia.” (7:38)

      • Ni nini kinachokuvutia kuhusu jitihada za Mashahidi wa Yehova za kuhubiri?

      Soma Mathayo 22:39 na Waroma 10:13-15, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Kazi yetu ya kuhubiri inaonyeshaje kwamba tunawapenda jirani zetu?

      • Yehova anahisije kuhusu wale wanaohubiri habari njema?​—Ona mstari wa 15.

  • Tunawezaje Kuwa Safi Machoni pa Mungu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 4. Shinda mazoea mabaya

      Mtu akitupa sigara kwenye kifaa cha kukusanya taka.

      Yehova anaweza kutusaidia kushinda zoea lolote baya

      Ikiwa wewe ni mraibu wa kuvuta sigara au kutumia dawa za kulevya, huenda unaelewa jinsi ilivyo vigumu kushinda mazoea hayo. Ni nini ambacho kitakusaidia? Fikiria madhara unayopata kutokana na mazoea hayo. Soma Mathayo 22:37-39, kisha mzungumzie jinsi kuvuta sigara au kutumia dawa za kulevya kunavyoathiri . . .

      • urafiki wa mtu na Yehova.

      • familia ya mtu huyo na watu wanaomzunguka.

      Chukua hatua ambazo zitakusaidia kushinda mazoea mabaya.a Onyesha VIDEO.

      VIDEO: Kuonyesha Sifa ya Kujizuia (2:47)

      Soma Wafilipi 4:13, kisha mzungumzie swali hili:

      • Kuwa na mazoea mazuri ya kusali, kujifunza Biblia, na kuhudhuria mikutano kunawezaje kumsaidia mtu apate nguvu za kushinda mazoea mabaya?

      5. Jitahidi kushinda mawazo na mazoea machafu

      Soma Wakolosai 3:5, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Tunajuaje kwamba kutazama ponografia, kutuma ujumbe au picha za ngono, na kupiga punyeto ni mazoea machafu machoni pa Yehova?

      • Je, inawezekana kufuata sheria za Yehova kuhusu usafi wa maadili? Kwa nini?

      Jifunze jinsi ya kushinda mawazo machafu. Onyesha VIDEO.

      VIDEO: Chukua Hatua ili Uendelee Kuwa Safi (1:51)

      Yesu alitoa mfano unaoonyesha kwamba tunapaswa kuchukua hatua thabiti ili tuendelee kudumisha maadili safi. Soma Mathayo 5:29, 30, kisha mzungumzie swali hili:

      • Ingawa Yesu hakumaanisha tunapaswa kujisababishia majeraha ya kimwili, alionyesha kwamba tunapaswa kuchukua hatua fulani. Mtu anapaswa kuchukua hatua gani thabiti ili kuepuka mawazo machafu?b

      Ikiwa unapambana ili kushinda mawazo machafu, Yehova anathamini jitihada zako. Soma Zaburi 103:13, 14, kisha mzungumzie swali hili:

      • Ikiwa unapambana na zoea chafu, andiko hili linawezaje kukusaidia uendelee kupambana?

      Usife moyo, endelea kupambana!

      Huenda ukajiambia hivi, ‘Nimeshindwa, hakuna haja ya kuendelea kupambana.’ Lakini fikiria jambo hili: Mkimbiaji anapoanguka haimaanishi kwamba hawezi kuendelea na mbio hizo, pia haimaanishi kwamba anapaswa kurudi nyuma na kuanza tena. Vivyo hivyo, hata unapolemewa na kurudia zoea hilo, haimaanishi kwamba huwezi kulishinda. Wala haimaanishi kwamba jitihada ulizofanya ni za bure. Ni jambo la kawaida kujikwaa. Lakini usife moyo! Kwa msaada wa Yehova, unaweza kushinda zoea baya.

      Mkimbiaji akisimama baada ya kuanguka.
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki