Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kizazi cha 1914 Kwa Nini ni cha Maana?
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Mei 1
    • Katika karne ya kwanza W.K., Yesu alisema kwamba kuwapo kwake kusikoonekana akiwa Mfalme mpya wa dunia kungeonyeshwa na ishara yenye kuonekana. Aliulizwa hivi: “Ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” Jibu lake likawa nini? “Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme, na kutakuwako upungufu wa chakula na matetemeko ya dunia mahali hapa na mahali hapa. Mambo hayo yote ni mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu.”—Mathayo 24:3, 7, 8, NW.

      Kulingana na hilo, vita iliyotokea katika 1914 iliandamana na upungufu wa chakula mbaya sana, kwa kuwa uzalishaji wa mazao ya chakula kulikatishwa kwa muda wa zaidi ya miaka minne. Vipi “matetemeko ya dunia mahali hapa na mahali hapa”? Katika mwongo uliofuata 1914, matetemeko ya dunia yenye uharibifu yasiyopungua kumi yaliua watu zaidi ya 350,000. (Ona sanduku.) Kwa kweli, kizazi cha 1914 kiliona “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu.” Na tangu wakati huo, maumivu makali ya ghafula ya taabu yamepiga kwa ukawaida kwa namna ya misiba-asilia, njaa, na vita vingi sana.

      Hata hivyo, habari ya kusimamishwa kwa Ufalme wa Mungu katika 1914 ni habari njema kwa sababu Ufalme huo utaokoa dunia hii kutoka uharibifu. Jinsi gani? Utaondoa dini zote bandia, za kinafiki, serikali zenye ufisadi, na uvutano mwovu wa Shetani. (Danieli 2:44; Warumi 16:20; Ufunuo 11:18; 18:4-8, 24) Isitoshe, utaleta ulimwengu mpya ambao “haki yakaa ndani yake.”—2 Petro 3:13.

      Upesi baada ya Vita ya Ulimwengu 1, Wanafunzi wa Biblia wenye mioyo myeupe, kama Mashahidi wa Yehova walivyojulikana wakati huo, walianza kutambua pendeleo lao kuhusu sehemu nyingine ya ishara ya kuwapo kwa Yesu akiwa Mfalme. Yesu Kristo alitabiri hivi: “Habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.”—Mathayo 24:14.

      Kutoka mianzo midogo katika 1919, Mashahidi wa Yehova wameendelea bila kuacha kueneza hizo “habari njema.” Likiwa tokeo, mamilioni kutoka nchi zaidi ya 200 sasa wanakusanywa kuwa raia wa Ufalme wa Mungu. Na ni mibaraka iliyoje inayowangojea raia hao! Ufalme huo utaondolea mbali vita, njaa, uhalifu, na uonevu. Utashinda hata ugonjwa na kifo!—Zaburi 46:9; 72:7, 12-14, 16; Mithali 2:21, 22; Ufunuo 21:3, 4.

      Kabla ya kizazi cha 1914 kupitilia mbali, kazi ya kuhubiri Ufalme itakuwa imetimiza kusudi layo. “Kwa kuwa,” akatabiri Yesu, “kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe. Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.”—Mathayo 24:21, 22.

  • Kizazi cha 1914 Kwa Nini ni cha Maana?
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Mei 1
    • [Chati katika ukurasa wa 7]

      MATETEMEKO YA DUNIA Katika Mwongo Uliofuata 1914

      Tarehe: Mahali: Vifo:

      Januari 13, 1915 Avezzano, Italia 32,600

      Januari 21, 1917 Bali, Indonesia 15,000

      Februari 13, 1918 Wilaya ya Kwangtung, Uchina 10,000

      Oktoba 11, 1918 Puerto Rico (magharibi) 116

      Januari 3, 1920 Veracruz, Meksiko 648

      Septemba 7, 1920 Reggio di Calabria, Italia 1,400

      Desemba 16, 1920 Wilaya ya Ningsia, Uchina 200,000

      Machi 24, 1923 Wilaya ya Szechwan, Uchina 5,000

      Mei 26, 1923 Iran (kaskazini-mashariki) 2,200

      Septemba 1, 1923 Tokyo-Yokohama, Japani 99,300

      Kutoka orodha ya “Matetemeko ya Dunia ya Maana ya Ulimwengu” katika kitabu Terra Non Firma cha James M. Gere na Haresh C. Shah.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki