-
Unabii wa Biblia Ambao Wewe Umeona UkitimizwaBiblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
-
-
25 Hata hivyo, Biblia yavuta fikira kwenye aina nyingine ya hayawani-mwitu ambaye amesababisha hofu kweli kweli katika miaka ya juzijuzi. Nabii Ezekieli alilinganisha binadamu wenye jeuri na wanyama aliposema: “Wakuu wake kati yake wamekuwa kama mbwa-mwitu wakirarua mawindo; ili kumwaga damu, na kuharibu roho [nafsi, NW] za watu, wapate faida kwa njia isiyo halali.” (Ezekieli 22:27) Alipotoa unabii juu ya “kuongezeka kwa kutokutii sheria,” kwa kweli, Yesu alikuwa akisema kwamba “hayawani-mwitu” hao wangekuwa wakichacha duniani wakati wa kuwapo kwake. (Mathayo 24:12, NW) Paulo mwandikaji wa Biblia aongeza kwamba katika “siku za mwisho” binadamu wangekuwa “wenye kupenda fedha . . . wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema.” (2 Timotheo 3:1-3) Je! imekuwa hivyo tangu 1914?
26-28. Ni ripoti zipi kuuzunguka ulimwengu zinazoonyesha kwamba “hayawani-mwitu” wahalifu wanaotea-otea duniani?
26 Hakika ndivyo. Ikiwa unaishi katika karibu jiji lolote kubwa la dunia, tayari wajua hilo. Lakini ikiwa unatia shaka, ebu fikiria manukuu ya magazeti ya juzijuzi yafuatayo. Kutoka Colombia: “Mwaka jana polisi waliandika . . . mauaji ya kukusudia karibu 10,000 na wizi wa kutumia silaha 25,000.” Kutoka Victoria, Australia: “Ongezeko Kubwa Katika Uhalifu Mkubwa.” Kutoka United States: “Machinjo Katika New York Yakaribia Hesabu Isiyopata Kufikiwa Tena.” “Detroit ilipita Gary, Indiana, mwaka jana kuwa jiji kubwa lenye hesabu ya mauaji mengi zaidi ya kukusudia katika taifa—58 kwa wakaaji 100,000.”
27 Kutoka Zimbabwe: “Kuua watoto kwa kukusudia kumefikia viwango vya kuhatarisha.” Kutoka Brazil: “Kuna uhalifu mwingi sana hapa, na matumizi mengi sana ya silaha, hivi kwamba habari za jeuri hazisisimui sana tena.” Kutoka New Zealand: “Mashambulizi ya kingono na uhalifu wenye jeuri waendelea kuwa hangaiko kubwa kwa polisi.” “Kiwango cha jeuri ya watu wa New Zealand kuelekeana chaweza kuelezwa tu kuwa ni unyama.” Kutoka Hispania: “Hispania yashindana na tatizo la uhalifu wenye kuongezeka.” Kutoka Italia: “Mafia wa Sicily, baada ya kudhoofika, wafufuka katika wimbi la mauaji.”
-
-
Unabii wa Biblia Ambao Wewe Umeona UkitimizwaBiblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
-
-
29, 30. Hali ya kidini katika Jumuiya ya Wakristo ikoje, katika kutimiza unabii wa Yesu?
29 Dini ingeendeleaje wakati wa msukosuko wa kuwapo kwa Yesu? Kwa upande mmoja, Yesu alitoa unabii kwamba kungekuwako ongezeko katika utendaji wa kidini: “Manabii wengi wa uwongo watatokea na kupotosha wengi.” (Mathayo 24:11, NW) Kwa upande mwingine, yeye alitabiri kwamba katika Jumuiya ya Wakristo yote, kupendezwa na Mungu kungeshuka sana. “Upendo wa wengi zaidi utapoa.”—Mathayo 24:12, NW.
30 Kwa kweli hilo laeleza yanayotukia leo katika Jumuiya ya Wakristo. Katika upande huu, makanisa makubwa yanashindwa kwa kukosa kuungwa mkono. Katika mabara ambayo wakati mmoja yalikuwa ya Kiprotestanti sana ya Ulaya na Uingereza, dini imekufa. Wakati uo huo, Kanisa Katoliki linaugua kwa kukosa makasisi na kwa upungufu wa kuungwa mkono. Kwa upande mwingine, kumekuwako maongezeko katika visehemu vya dini ndogo. Vidhehebu vyenye kutegemea dini za Nchi za Mashariki vinavuvumuka sana, huku wainjilisti wa televisheni wenye pupa wakinyonya watu mamilioni ya dola.
-