-
“Ni Nini Itakayokuwa Ishara ya Kuwapo Kwako?”Mnara wa Mlinzi—1994 | Februari 15
-
-
“NDIPO” Mwisho
10. Kwa nini tuchunguze neno la Kigiriki toʹte, na umaana walo ni nini?
10 Katika sehemu fulani za unabii wake Yesu alionyesha matukio yakitokea kwa kufuatana. Yeye alisema hivi: “Habari njema ya ufalme itahubiriwa . . . hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.” Mara nyingi Biblia mbalimbali hutumia neno “ndipo” zikiwa na maana sahili ya kusema “kwa hiyo” au “lakini.” (Marko 4:15, 17; 13:23) Hata hivyo, kwenye Mathayo 24:14, “ndipo” linategemea kielezi cha Kigiriki to΄te.c Wataalamu wa Kigiriki waeleza kwamba to΄te ni “kielezi-kionyeshi cha wakati” kinachotumiwa “kujulisha yale yanayofuata katika wakati” au “kujulisha tukio lifuatalo.” Hivyo Yesu alitabiri kwamba kungekuwa na kuhubiriwa kwa Ufalme na ndipo (‘baada ya hilo’ au, ‘kufuatia hilo’) “mwisho” ungekuja. Mwisho gani?
-
-
“Ni Nini Itakayokuwa Ishara ya Kuwapo Kwako?”Mnara wa Mlinzi—1994 | Februari 15
-
-
c Toʹte huonekana zaidi ya mara 80 katika Mathayo (mara 9 katika sura ya 24) na mara 15 katika kitabu cha Luka. Marko alitumia toʹte mara sita pekee, lakini mara nne kati yazo zilihusisha “ishara.”
-