Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kubaki Tukiwa Tumejipanga Kitengenezo Ili Tuokoke Kuingia Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Septemba 1
    • 6. (a) Uzawa wa Ufalme ulitaka kazi gani iliyotabiriwa na Yesu? (b) Kufanya kazi hii kulitaka nini kwa upande wa watu wa Yehova, na ni kabiliano la namna gani wanalotokeza sasa?

      6 Uzawa wa Ufalme wa Yehova ambao kupitia kwao atatetea uhaki wake wa enzi kuu juu ya ulimwengu wote mzima—aha, hapa kukawa na jambo fulani lililostahili kutangazwa duniani pote! Na hapa kukawa na wakati wa kutimiza maneno haya ya Yesu kuhusu uthibitisho wa “kuwapo” kwake kusikoonekana: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.” (Mathayo 24:3, 14, NW) Kuhubiri kwa umoja na upatani duniani pote hakika kungetaka kupanga kitengenezo sehemu ionekanayo ya tengenezo la Yehova la ulimwengu wote mzima. Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti, kama ilivyowakilishwa na msimamizi wayo wa wakati huo, J. F. Rutherford, ilipendelea kufanya hivyo. Kwa hiyo kuanzia mwaka wa 1919 baada ya vita, kupangwa kitengenezo kwa waunga mkono washikamanifu wa Sosaiti wakiwa taifa lililorudishwa kuliendelea mbele kwa kupiga moyo konde, pamoja na sala ya mwongozo na baraka ya Mtengeneza Mambo Mkuu Zaidi, Yehova Mungu. Wajapopatwa na upinzani mkali wa Wafashisti, harakati ya Nazi ya Hitler, Aksio ya Wakatoliki na kukabiliwa na Vita ya Ulimwengu 2, Mashahidi wa Yehova duniani pote walielekeana na ulimwengu wenye uadui wakiwa na umoja.

  • Kubaki Tukiwa Tumejipanga Kitengenezo Ili Tuokoke Kuingia Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Septemba 1
    • 9. Kwa nini kondoo wanaalikwa warithi ‘ufalme waliowekewa tayari,’ na ni kwa njia gani wamo katika hali nzuri zaidi kuwatendea mema ndugu za Mfalme?

      9 Kwa nini watu hawa wa aina ya kondoo waalikwa ‘waurithi ufalme waliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu’? Mfalme awaambia kwamba ni kwa sababu wamewatendea “ndugu” zake mema, na kwa sababu hiyo walimtendea yeye. Kwa usemi “ndugu,” Mfalme anamaanisha mabaki wa ndugu zake wa kiroho ambao wangali duniani katika umalizio huu wa mfumo wa mambo. Wakiisha kuwa kundi moja na akina ndugu wa Mchungaji-Mfalme, Yesu Kristo, wangeshirikiana kwa ukaribu sana iwezekanavyo pamoja na mabaki wa hao na kwa hiyo wangekuwa katika hali nzuri kabisa ya kuwatendea mema. Hata katika njia za kimwili, wangewasaidia ndugu za Yesu kuhubiri ulimwenguni pote ujumbe wa Ufalme uliosimamishwa kabla mwisho haujaja. Kwa sababu hii, kondoo wangehazini pendeleo lao la kuwa wamepangwa kitengenezo pamoja na mabaki wakiwa kundi moja la Mchungaji mmoja.

  • Kubaki Tukiwa Tumejipanga Kitengenezo Ili Tuokoke Kuingia Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Septemba 1
    • 11. Kondoo wanaonyeshaje kwamba wao wanatetea Ufalme, na kwa sababu ya hilo, ni baraka gani ambayo ni yao?

      11 Kwa kutofautiana na mbuzi wa mfano, watu wa aina ya kondoo wanaonyesha kwamba wanatetea Ufalme waziwazi. Jinsi gani? Kwa vitendo, si maneno matupu tu. Kwa sababu ya kutoonekana kwa Mfalme katika mbingu, hawawezi kumtendea mema moja kwa moja kwa kuunga mkono Ufalme wake. Kwa hiyo wanawatendea mema ndugu zake wa kiroho ambao bado wako duniani. Ijapokuwa hilo linatokeza chuki, upinzani, na mnyanyaso kutoka kwa mbuzi, kwa sababu ya huko kutenda mema, kondoo wanaambiwa na Mfalme kwamba ndio ‘waliobarikiwa na Baba yake.’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki