-
Utasimamaje Mbele ya Kiti cha Hukumu?Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
-
-
20, 21. Mitume wa Yesu waliuliza nini kinachohusu wakati wetu, kikitokeza swali gani?
20 Muda mfupi kabla ya Yesu kufa, mitume wake walimwuliza hivi: “Mambo haya yatakuwa wakati gani, nayo ni nini itakuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” (Mathayo 24:3, NW) Yesu alitabiri matukio muhimu ambayo yangetokea duniani kabla ya ‘mwisho kuja.’ Muda mfupi kabla ya mwisho huo, mataifa “yatamwona Mwana wa binadamu akija juu ya mawingu ya mbinguni na nguvu na utukufu mkubwa.”—Mathayo 24:14, 29, 30, NW.
21 Lakini, itakuwaje kwa watu katika mataifa hayo Mwana wa binadamu afikapo katika utukufu wake? Ebu tuone kutokana na mfano wa kondoo na mbuzi, unaoanza kwa maneno haya: “Wakati Mwana wa binadamu awasilipo katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu. Na mataifa yote yatakusanywa mbele yake.”—Mathayo 25:31, 32, NW.
22, 23. Ni mambo yapi yaonyeshayo kwamba mfano wa kondoo na mbuzi haukuanza kutimizwa katika 1914?
22 Je, mfano huu unahusu wakati Yesu alipoketi katika mamlaka ya kifalme katika 1914, kama ambavyo tumeelewa kwa muda mrefu? Naam, Mathayo 25:34 lasema juu yake akiwa Mfalme, kwa hiyo kwa kupatana na akili mfano huu wahusu tangu wakati Yesu alipokuwa Mfalme katika 1914. Lakini ni hukumu gani aliyofanya upesi baadaye? Haikuwa hukumu ya “mataifa yote.” Badala ya hivyo, alielekeza uangalifu wake kwa wale wanaodai kufanyiza “nyumba ya Mungu.” (1 Petro 4:17, italiki ni zetu.) Kwa kupatana na Malaki 3:1-3, Yesu, akiwa mjumbe wa Yehova, alikagua kihukumu Wakristo watiwa-mafuta waliosalia duniani. Pia ulikuwa wakati wa kutoa adhabu ya kihukumu juu ya Jumuiya ya Wakristo, waliodai kwa uwongo kuwa “nyumba ya Mungu.”c (Ufunuo 17:1, 2; 18:4-8) Lakini hakuna chochote kionyeshacho kwamba wakati huo, au tangu wakati huo, Yesu aliketi ili kuhukumu watu wa mataifa yote hatimaye kuwa kondoo au mbuzi.
23 Tukichanganua utendaji wa Yesu katika mfano huu, twamwona hatimaye akihukumu mataifa yote. Mfano huu hauonyeshi kwamba kuhukumu huko kungeendelea kwa kipindi kirefu cha miaka mingi, kana kwamba kila mtu aliyekufa katika miongo hii ambayo imepita alihukumiwa kustahili kifo kidumucho milele au uhai udumuo milele. Yaonekana kwamba wengi ambao wamekufa katika miongo ya majuzi wameenda katika kaburi la kawaida la wanadamu. (Ufunuo 6:8; 20:13) Hata hivyo, huu mfano waonyesha wakati ambapo Yesu ahukumu watu wa “mataifa yote” ambao wakati huo wako hai na wanakabili utekelezaji wa adhabu yake ya kihukumu.
24. Ni lini mfano wa kondoo na mbuzi utakapotimizwa?
24 Kwa maneno mengine, mfano huu waelekezea wakati ujao ambapo Mwana wa binadamu atakuja katika utukufu wake. Ataketi ili kuhukumu watu wanaoishi wakati huo. Hukumu yake itategemea kile ambacho wamejidhihirisha wenyewe kuwa. Wakati huo ‘upambanuzi kati ya wenye haki na waovu’ utakuwa umethibitishwa wazi. (Malaki 3:18) Kule kutangaza hasa na kutekeleza hukumu kutafanywa kwa kipindi kifupi. Yesu atatoa maamuzi yenye haki yanayotegemea yale ambayo watu mmoja-mmoja watakuwa wamedhihirisha wazi.—Ona pia 2 Wakorintho 5:10.
25. Mathayo 25:31 laonyesha nini likisema juu ya Mwana wa binadamu akiketi katika kiti cha utukufu?
25 Basi, hii yamaanisha kwamba ‘kuketi kwa Yesu katika kiti chake cha utukufu’ ili kutoa hukumu, kunakotajwa katika Mathayo 25:31, kwahusu wakati ujao wakati Mfalme huyu mwenye nguvu atakapoketi kutangaza na kutekeleza hukumu dhidi ya mataifa. Ndiyo, mandhari ya hukumu inayohusu Yesu katika Mathayo 25:31-33, 46 yalingana na mandhari iliyo katika Danieli sura ya 7, ambamo Mfalme anayetawala, Mkale wa Siku, aliketi ili kutekeleza fungu lake akiwa Hakimu.
26. Ni maelezo gani mapya ya huu mfano yanayodhihirika?
26 Kuelewa huu mfano wa kondoo na mbuzi kwa njia hii kwaonyesha kwamba kutoa hukumu juu ya kondoo na mbuzi ni kwa wakati ujao. Kutatokea baada ya “dhiki” inayotajwa katika Mathayo 24:29, 30 kufyatuka na Mwana wa binadamu ‘kufika katika utukufu wake.’ (Linganisha Marko 13:24-26, NW.) Ndipo, mfumo huu wote ukiwa umefikia mwisho wao, Yesu atafanya mahakama na kutoa na kutekeleza hukumu.—Yohana 5:30; 2 Wathesalonike 1:7-10.
-
-
Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
-
-
3. Mapema katika maneno yake, Yesu alisema nini kingetukia mara tu baada ya dhiki kubwa kuanza?
3 Yesu alitabiri matukio makubwa ambayo yangetukia “mara baada ya” kufyatuka kwa dhiki kubwa, matukio tunayongoja. Alisema kwamba ndipo “ishara ya Mwana wa binadamu” itatokea. Hili litaathiri kabisa “makabila yote ya dunia” ambayo “yatamwona Mwana wa binadamu akija juu ya mawingu ya mbinguni na nguvu na utukufu mkubwa.” Mwana wa binadamu ataandamana na “malaika zake.” (Mathayo 24:21, 29-31, NW)a Vipi juu ya mfano wa kondoo na mbuzi? Biblia za kisasa huuweka katika sura ya 25, lakini huo ni sehemu ya jibu la Yesu, ukieleza mambo mengine zaidi kuhusu kuja kwake katika utukufu na kukazia hukumu yake juu ya “mataifa yote.”—Mathayo 25:32, NW.
Wahusika Katika Huu Mfano
4. Mfano wa kondoo na mbuzi wataja nini mwanzoni kuhusu Yesu, na ni nani pia wanaotajwa?
4 Yesu aanza huu mfano kwa kusema: “Wakati Mwana wa binadamu awasilipo.” Yaelekea unajua “Mwana wa binadamu” ni nani. Waandikaji wa Gospeli mara nyingi walitumia usemi huo kumhusu Yesu. Hata Yesu mwenyewe aliutumia hivyo, bila shaka akikumbuka ono la Danieli la “mtu kama mwana wa binadamu” akimwendea Mkale wa Siku ili kupokea “utawala na heshima na ufalme.” (Danieli 7:13, 14, NW; Mathayo 26:63, 64, NW; Marko 14:61, 62, NW) Ingawa Yesu ndiye mhusika-mkuu katika mfano huu, hayuko peke yake. Mapema katika maneno yake, kama yalivyonukuliwa katika Mathayo 24:30, 31, alisema kwamba Mwana wa binadamu ‘ajapo na nguvu na utukufu mkubwa,’ malaika zake watatimiza fungu muhimu. Vivyo hivyo, mfano wa kondoo na mbuzi waonyesha malaika wakiwa na Yesu aketipo ‘juu ya kiti cha ufalme chenye utukufu’ ili kuhukumu. (Linganisha Mathayo 16:27.) Lakini Hakimu na malaika zake wako mbinguni, basi, je, wanadamu wanazungumzwa katika huu mfano?
-
-
Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
-
-
ONA MILINGANO
Mathayo 24:29-31, NW Mathayo 25:31-33, NW
Baada ya dhiki kubwa Mwana wa binadamu yuaja
kuanza, Mwana wa binadamu awasili
Yuaja na utukufu mkubwa Awasili katika utukufu na kuketi katika
kiti chake cha ufalme chenye utukufu
-
-
Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
-
-
Makabila yote ya dunia Mataifa yote yakusanywa; mbuzi wahukumiwa
yamwona hatimaye (dhiki kubwa yaisha)
-