Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?
    Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
    • 4. Mfano wa kondoo na mbuzi wataja nini mwanzoni kuhusu Yesu, na ni nani pia wanaotajwa?

      4 Yesu aanza huu mfano kwa kusema: “Wakati Mwana wa binadamu awasilipo.” Yaelekea unajua “Mwana wa binadamu” ni nani. Waandikaji wa Gospeli mara nyingi walitumia usemi huo kumhusu Yesu. Hata Yesu mwenyewe aliutumia hivyo, bila shaka akikumbuka ono la Danieli la “mtu kama mwana wa binadamu” akimwendea Mkale wa Siku ili kupokea “utawala na heshima na ufalme.” (Danieli 7:13, 14, NW; Mathayo 26:63, 64, NW; Marko 14:61, 62, NW) Ingawa Yesu ndiye mhusika-mkuu katika mfano huu, hayuko peke yake. Mapema katika maneno yake, kama yalivyonukuliwa katika Mathayo 24:30, 31, alisema kwamba Mwana wa binadamu ‘ajapo na nguvu na utukufu mkubwa,’ malaika zake watatimiza fungu muhimu. Vivyo hivyo, mfano wa kondoo na mbuzi waonyesha malaika wakiwa na Yesu aketipo ‘juu ya kiti cha ufalme chenye utukufu’ ili kuhukumu. (Linganisha Mathayo 16:27.) Lakini Hakimu na malaika zake wako mbinguni, basi, je, wanadamu wanazungumzwa katika huu mfano?

  • Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?
    Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
    • Malaika wako pamoja naye Malaika wawasili pamoja naye

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki