Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Ufalme Wako na Uje”
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
    • 15, 16. Maneno “kizazi hiki” yanarejelea nani?

      15 Hata hivyo, Ufalme wa Mungu utakuja lini? Yesu hakutaja wakati hususa ambao Ufalme huo ungekuja. (Mt. 24:36) Lakini alisema jambo fulani ambalo linapaswa kutuhakikishia kwamba Ufalme huo uko karibu sana. Yesu alisema kwamba Ufalme ungekuja baada ya “kizazi hiki” kushuhudia utimizo wa ishara ya unabii. (Soma Mathayo 24:32-34.) Maneno “kizazi hiki” yanarejelea nani? Acheni tuchunguze kwa makini maneno hayo ya Yesu.

      16 “Kizazi hiki.” Je, Yesu alikuwa akirejelea watu wasioamini? Hapana. Fikiria wasikilizaji wake. Yesu alitoa unabii huo kwa mitume wake wachache ambao ‘walimkaribia faraghani.’ (Mt. 24:3) Punde si punde mitume wangetiwa mafuta kwa roho takatifu. Fikiria pia muktadha. Kabla hajasema kuhusu “kizazi hiki,” Yesu alisema: “Basi jifunzeni jambo hili kutokana na mtini kama mfano: Mara tu tawi lake changa linapokuwa jororo na kutoa majani, mnajua kwamba kiangazi kiko karibu. Vivyo hivyo ninyi pia, mnapoona mambo yote hayo, jueni kwamba yuko karibu milangoni.” Wafuasi wa Yesu waliotiwa mafuta—na si watu wasioamini—ndio wangeona mambo ambayo Yesu alitabiri na kutambua maana yake, yaani, kwamba Yesu “yuko karibu milangoni.” Kwa hiyo, Yesu aliposema kuhusu “kizazi hiki,” alikuwa akirejelea wafuasi wake watiwa-mafuta.

      KIZAZI

      (Mt. 24:32-34)

      Yesu alionyesha kwamba Ufalme utakuja baada ya “kizazi hiki” kushuhudia utimizo wa ishara ya unabii (Ona fungu la 17, 18)

      Chati ya “kizazi hiki” kutoka kwa mfano wa Yesu katika Mathayo 24:32-34

      KIKUNDI CHA 1: Watiwa-mafuta ambao waliona mwanzo wa utimizo wa ile ishara katika mwaka wa 1914

      KIKUNDI CHA 2: Watiwa-mafuta ambao waliishi wakati mmoja na wale wa kikundi cha kwanza, baadhi yao wataiona dhiki kuu

      17. Maneno “kizazi” na “mambo yote hayo” yanamaanisha nini?

      17 “Hakitapitilia mbali kamwe mpaka mambo yote hayo yatukie.” Maneno hayo yatatimiaje? Ili kujibu swali hilo, tunahitaji kujua mambo mawili: maana ya “kizazi” na “mambo yote hayo.” Neno “kizazi” mara nyingi hurejelea watu wenye umri mbalimbali ambao maisha yao yanapishana katika kipindi fulani hususa cha wakati. Kizazi si kipindi kirefu sana, na kina mwisho. (Kut. 1:6) Maneno “mambo yote hayo” yanatia ndani matukio yote yaliyotabiriwa kwamba yangetukia wakati wa kuwapo kwa Yesu, kulikoanza mwaka wa 1914 na kutamalizika wakati wa “dhiki kuu.”—Mt. 24:21.

      18, 19. Tunaweza kuelewaje maneno ya Yesu kuhusu “kizazi hiki,” na tunaweza kufikia mkataa gani?

      18 Hivyo basi, tueleweje maneno ya Yesu kuhusu “kizazi hiki”? Kizazi hicho kinafanyizwa na vikundi viwili vya watiwa-mafuta ambao maisha yao yanapishana. Kikundi cha kwanza kinafanyizwa na watiwa-mafuta ambao waliona mwanzo wa utimizo wa ile ishara katika mwaka wa 1914 na kikundi cha pili kinafanyizwa na watiwa-mafuta ambao kwa muda fulani waliishi wakati mmoja na wale wa kikundi cha kwanza. Angalau baadhi ya watiwa-mafuta walio katika kikundi cha pili wataona mwanzo wa dhiki kuu inayokuja. Vikundi vyote viwili vinafanyiza kizazi kimoja kwa sababu maisha yao wakiwa Wakristo watiwa-mafuta yanapishana kwa muda fulani.c

      19 Tunaweza kufikia mkataa gani? Tunajua kwamba ishara ya kuwapo kwa Yesu katika mamlaka ya Kifalme inaonekana wazi ulimwenguni pote. Pia, tunaona kwamba watiwa-mafuta ambao bado wako hai na ni sehemu ya “kizazi hiki” wanaendelea kuzeeka; hata hivyo, hawatakufa wote kabla ya dhiki kuu kuanza. Hivyo basi, tunaweza kufikia mkataa kwamba hivi karibuni pasipo shaka Ufalme wa Mungu utakuja na kutawala juu ya dunia! Itasisimua sana kuona utimizo wa sala tuliyofundishwa na Yesu: “Ufalme wako na uje”!

  • “Ufalme Wako na Uje”
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki