-
“Tuambie, Mambo Haya Yatakuwa Wakati Gani?”Mnara wa Mlinzi—2013 | Julai 15
-
-
16. Kuja kwa Yesu kunatajwa katika maandiko gani mengine?
16 Kuhusu mtumwa mwaminifu na mwenye busara, Yesu alisema hivi: “Mtumwa huyo atakuwa mwenye furaha ikiwa bwana wake atakapofika atamkuta akifanya hivyo.” Katika mfano wake wa mabikira, Yesu alisema hivi: “Walipokuwa wakienda zao kununua, bwana-arusi akafika [“akaja,” Kingdom Interlinear].” Katika mfano wa talanta, Yesu anasimulia hivi: “Baada ya muda mrefu bwana wa watumwa hao alikuja.” Katika mfano huohuo, bwana anasema hivi: “Wakati wa kufika kwangu [“kuja,” Int] ningekuwa nikipokea kilicho changu.” (Mt. 24:46; 25:10, 19, 27) Kuja kwa Yesu katika pindi hizo nne kunatukia wakati gani?
17. Tulisema nini kuhusu kufika kunakotajwa katika Mathayo 24:46?
17 Zamani, tulitaja katika machapisho yetu kwamba marejeo hayo manne ya mwisho yanahusu kufika, au kuja, kwa Yesu katika mwaka wa 1918. Kwa mfano, fikiria maneno ya Yesu kuhusu “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Soma Mathayo 24:45-47.) Tulielewa kwamba ‘kufika’ kunakotajwa katika mstari wa 46 kulihusiana na wakati ambapo Yesu alikuja kukagua hali ya kiroho ya watiwa-mafuta katika mwaka wa 1918 na mtumwa aliwekwa rasmi juu ya mali zote za Bwana katika mwaka wa 1919. (Mal. 3:1) Hata hivyo, uchunguzi zaidi wa unabii wa Yesu unaonyesha kwamba tunahitaji kurekebisha uelewaji wetu kuhusu wakati wa kutimia kwa mambo fulani yaliyo katika unabii huo wa Yesu. Kwa nini?
18. Kuchunguza unabii wote wa Yesu kunatufanya tufikie mkataa gani kuhusu kuja kwa Yesu?
18 Katika mistari inayotangulia Mathayo 24:46, neno “atakuja” linatumiwa kila mara kurejelea wakati ambapo Yesu atakuja kutangaza na kutekeleza hukumu wakati wa dhiki kuu. (Mt. 24:30, 42, 44) Pia, kama tulivyoona katika fungu la 12, ‘kufika’ kwa Yesu kunakotajwa katika Mathayo 25:31 kunarejelea wakati huohuo ujao wa hukumu. Kwa hiyo, ni jambo linalopatana na akili kufikia mkataa kwamba kufika kwa Yesu ili kumweka rasmi mtumwa mwaminifu juu ya mali zake zote kunakotajwa katika Mathayo 24:46 na 47, kunahusu pia kuja kwake wakati ujao, wakati wa ile dhiki kuu.f Kwa kweli, kuchunguza unabii wote wa Yesu kunaonyesha wazi kwamba kila moja ya marejeo hayo manane kuhusu kuja kwake, yatatimia wakati ujao wa hukumu katika ile dhiki kuu.
-
-
“Tuambie, Mambo Haya Yatakuwa Wakati Gani?”Mnara wa Mlinzi—2013 | Julai 15
-
-
e Fungu la 15: Maneno “atakuja” na “atafika” yametafsiriwa kutokana na kitenzi kilekile cha Kigiriki, erʹkho·mai.
f Fungu la 18: Kama ilivyoonyeshwa, neno la Kigiriki linalotafsiriwa “atakapofika” katika Mathayo 24:46 ni kitenzi kilekile cha Kigiriki kinachotafsiriwa “atakuja” katika Mathayo 24:30, 42, 44.
-