-
Wale Wanawali Wenye Hekima na WapumbavuMnara wa Mlinzi—1990 | Aprili 15
-
-
Ukawivu mwendelevu wa bwana-arusi huonyesha kwamba kuwapo kwa Kristo akiwa Mfalme anayetawala kungekuwa katika wakati ujao ulio mbali. Hatimaye anakuja kwenye kiti chake cha ufalme katika mwaka 1914. Wakati wa ule usiku mrefu kabla ya hapo, wale wanawali wote wanalala usingizi. Lakini hawakushutumiwa kwa sababu hiyo. Wale wanawali wapumbavu wanashutumiwa kwa kutokuwa na mafuta kwa ajili ya vyombo vyao. Yesu aeleza namna wale wanawali wanavyoamka kabla ya bwana-arusi kuwasili:
“Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki. Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao. Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika. Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.”
-
-
Wale Wanawali Wenye Hekima na WapumbavuMnara wa Mlinzi—1990 | Aprili 15
-
-
Baada ya Kristo kuwasili katika Ufalme wake wa kimbingu, jamii ya wale wanawali wenye busara ya Wakristo wa kweli wapakwa-mafuta waliamuka kwenye pendeleo lao la kuangaza nuru katika ulimwengu huu uliotiwa giza katika kusifu Bwana-arusi aliyerudi. Lakini wale waliofananishwa na wale wanawali wapumbavu walikuwa hawako tayari kuandaa sifa hii ya kukaribisha. Kwa hiyo wakati ufikapo, Kristo hawafungulii mlango wa karamu ya arusi mbinguni. Yeye awaacha nje katika weusi wa usiku mzito zaidi ya wote wa ulimwengu, wakapotee na wafanya kazi wengine wote wa uasi-sheria. “Basi kesheni,” Yesu amalizia, “kwa sababu hamjui siku wala saa.” Mathayo 25:1-13.
-