-
Nuru ya Elimu Wakati wa “Umalizio wa Mfumo wa Mambo”Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
-
-
13. Wanawali wenye akili waliitikiaje ombi la wale wanawali wapumbavu?
13 Namna gani, sasa, juu ya wale wapumbavu wa jamii ya wanawali? Yesu anaendelea kusema hivi: “Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika. Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.”—Mathayo 25:8, 9.
-
-
Nuru ya Elimu Wakati wa “Umalizio wa Mfumo wa Mambo”Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
-
-
15. (a) Wakati kipindi chenye amani kilipoanza, ni nani kati ya jamii ya wanawali walioanza kuonyesha maelekeo ya upumbavu wa kiroho? (b) Kwa sababu gani wale wanawali wenye akili hawakuweza kuwasaidia wale wanawali waliokuwa wapumbavu kiroho?
15 Kile kipindi cha amani kilipokuwa kinaanza, baadhi ya wale waliodai kuwa washiriki walio wakfu na kubatizwa, walianza kuonyesha upumbavu wa kiroho. Baada ya kifo cha msimamizi wa kwanza wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, Charles Taze Russell, hawakuingia kabisa kwenye roho ya matukio pamoja na chombo kionekanacho cha Yehova Mungu chini ya msimamizi wacho mpya, J. F. Rutherford. Mioyo yao haikupatana kabisa na namna mambo yalivyokuwa yakifanywa. Walionyesha ukosefu wa kuthamini namna Yehova alivyokuwa akishughulika na watu wake. Hivyo, wale waliokuwa kama wanawali wenye akili hawangeweza kutia roho ya ushirikiano wa kutoka moyoni katika hao wapumbavu waliokuwa wakijitenga wenyewe zaidi na zaidi.
16. Upumbavu wa kiroho ulifanywaje uonekane kwa upande wa wale wanawali wapumbavu?
16 Kwa njia hiyo upumbavu wa kiroho ulifanywa uonekane. Namna gani? Kupitia kushindwa kuwa na yale mafuta ya mfano wakati huo wa maana sana kulipokuwa na uhitaji mkubwa wa nuru ya elimu ya kiroho kadiri matukio mapya yalivyosonga mbele, yakionyesha kwamba yule Bwana-arusi alikuwapo. Kwa hiyo ulikuwa ni wakati wa kutoka nje kumlaki na taa ya mtu ikiwa imewashwa na kuangaza kabisa, kwa njia ya mfano. Lakini badala yake, wale waliofanana na wanawali wapumbavu, ambao taa zao zilikuwa zinazimika, waliachana na wale waliokuwa wenye akili.
-