Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uongozi Wenye Kutenda wa Kristo Leo
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Agosti 1
    • 1. Ni katika njia gani Kristo alikabidhi “mali” zake kwa wanafunzi wake?

      WAKATI Kristo alipokaribia kuwaacha wanafunzi wake na kurudi mbinguni katika 33 W.K., yeye ‘aliweka kwao mali zake.’ Hilo lilihusu kuwa “mabalozi badala ya Kristo” na kuchukua kazi ya kuhubiri aliyokuwa ameanza, wakiieneza kufika “sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” Kabla ya kuwaacha, yeye alikuwa amewaagiza ‘wafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.’ Je! sisi tuna ushuhuda wa kwamba yeye alikuwa mwangalifu kuona jinsi walivyokuwa wakitekeleza utume huu? Kweli kweli tunao!—Mathayo 25:14; 2 Wakorintho 5:20, NW; Matendo 1:8, NW; Mathayo 28:19, NW.

  • Uongozi Wenye Kutenda wa Kristo Leo
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Agosti 1
    • Bwana na Mtumwa Wake

      4. Kristo ‘alisafiri’ ng’ambo jinsi gani na kisha akarudi “baada ya siku nyingi”?

      4 Baada ya yeye kujifananisha na “mtu atakaye kusafiri, [aliyeita] watumwa wake, akaweka kwao mali zake,” Kristo aliongeza hivi: “Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao.” (Mathayo 25:14, 19) Katika 33 W.K. Kristo ‘alikwenda zake mbinguni,’ alipoketishwa kwenye “mkono wa kuume wa Mungu.” (1 Petro 3:22) “Baada ya siku nyingi,” kufuatia kutawazwa kwake katika 1914, Kristo alianza ‘kutiisha katikati ya adui zake.’ Kwa kumvurumisha Shetani na mashetani zake chini kwenye dunia. (Zaburi 110:1, 2, NW; Ufunuo 12:7-9) Ndipo alipoelekeza fikira zake kwa watumwa wake. Wakati ulikuwa umefika wa kufanya hesabu pamoja nao. Zaidi ya wakati mwingine wo wote, yeye alikuwa ndiye Kiongozi wao mwenye kutenda.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki