Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kufanya Hesabu Juu ya Matumizi ya Hazina za Kristo
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
    • 1. Ni serikali gani ambayo haina matatizo ya kiuchumi, na ni nani ambao sasa lazima watoe hesabu kwa serikali hiyo?

      HAKUNA serikali isiyo na matatizo ya kiuchumi, isipokuwa moja tu. Serikali nyingi zina madeni makubwa. Ile serikali moja ambayo haina matatizo ya kiuchumi ni “ufalme wa mbinguni” ambao sasa umetangazwa kwa mapana na marefu. (Mathayo 25:1) Duniani wangali wapo wale wanaotazamiwa kuwa washiriki wa Ufalme huo wa kimbingu wanaotumikia serikali hiyo. Katika kipindi hiki chenye hatari sana cha historia yote ya kibinadamu, watumishi hao wa “ufalme wa mbinguni” wanaitwa watoe hesabu. Lazima wafanye hesabu na serikali hiyo kwa habari ya namna wametumia vitu vyenye thamani walivyokabidhiwa.

      2. Kwa sababu gani inatupasa tupendezwe sana na mfano fulani uliotolewa na “Mwana-Mfalme wa Amani”?

      2 Ili kuonyesha mfano wa jambo hilo, yule mwakilishi mwenye kutokeza zaidi wa huo “ufalme wa mbinguni” zamani sana alitoa mfano. Huo unapasa utupendeze leo, kwa sababu yule “Mwana-Mfalme wa Amani” aliutia katika unabii wake wenye kufika mbali kuhusu “ishara” ambayo ingetia alama “kuwapo” kwake katika Ufalme akiwa na uwezo kamili wa kutawala. (Mathayo 24:3, NW) Sisi leo hatuwezi kuepuka matokeo yatakayofuata kutimizwa kwa mfano huu wa kiunabii, kwa kuwa kuendelea kuwapo kwetu, maisha zetu zenyewe, zinahusika. Kwa hiyo, sasa, hivi ndivyo yule “Mwana-Mfalme wa Amani” alivyosimulia mfano huo kwa mitume wake siku chache tu kabla ya kifo chake cha dhabihu huko Kalvari.

  • Kufanya Hesabu Juu ya Matumizi ya Hazina za Kristo
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
    • 3. Wale watumwa waliopokea talanta kutoka kwa bwana-mkubwa kabla ya kuondoka walizitumiaje wakati wa kutokuwapo kwake?

      3 “Basi kesheni [endeleeni kulinda, NW], kwa sababu hamwijui siku wala saa. Maana ni mfano wa mtu atakaye kusafiri, aliwaita watumwa wake, akaweka kwao mali zake. Akampa mmoja talantaa tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri. Mara yule aliyepokea talanta tano akaenda, akafanya biashara nazo, akachuma faida talanta nyingine tano. Vilevile na yule mwenye mbili, yeye naye akachuma nyingine mbili faida. Lakini yule aliyepokea moja alikwenda akafukua chini, akaificha fedha ya bwana wake.

  • Kufanya Hesabu Juu ya Matumizi ya Hazina za Kristo
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
    • 6 “Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi. Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa. Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.”—Mathayo 25:13-30.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki