-
Ni Nini Hukuchochea Kumtumikia Mungu?Mnara wa Mlinzi—1995 | Juni 15
-
-
17. Katika maneno yako mwenyewe, eleza kifupi mfano wa talanta.
17 Ebu fikiria mfano wa Yesu wa talanta, kama ulivyorekodiwa kwenye Mathayo 25:14-30. Mtu mmoja aliyekuwa karibu kusafiri mbali aliwaita watumwa wake na kuwapa mali zake. “Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake.” Bwana-mkubwa aliporudi kutoza hesabu watumwa wake, alipata nini? Mtumwa aliyekuwa amepewa talanta tano alipata talanta tano zaidi. Vivyo hivyo, mtumwa aliyekuwa amepewa talanta mbili alipata talanta mbili zaidi. Mtumwa aliyekuwa amepewa talanta moja aliizika ardhini naye hakufanya lolote ili kuongeza mali ya bwana-mkubwa wake. Bwana-mkubwa alichanganuaje hali hiyo?
18, 19. (a) Kwa nini bwana-mkubwa hakumlinganisha mtumwa aliyepewa talanta mbili na yule aliyepewa talanta tano? (b) Mfano wa talanta watufundisha nini kuhusu pongezi na milinganisho? (c) Kwa nini mtumwa wa tatu alipata hukumu ya adhabu?
18 Kwanza, ebu tufikirie mtumwa aliyepewa talanta tano na yule aliyepewa talanta mbili. Kwa kila mmoja wao, bwana-mkubwa alisema: “Vema, mtumwa mwema na uaminifu.” Je, angemwambia hivyo mtumwa mwenye talanta tano kama mtumwa huyo angepata talanta mbili tu? Haielekei hivyo! Kwa upande mwingine, hakumwambia mtumwa aliyepata talanta mbili: ‘Kwa nini hukupata talanta tano? Ona mtumwa mwenzako na jinsi alivyopata nyingi kwa niaba yangu!’ La, bwana-mkubwa mwenye huruma-nyororo, aliyefananisha Yesu, hakuwalinganisha. Yeye aliwapa talanta “kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake,” naye hakutarajia kupata zaidi ya uwezo wa kila mmoja wao. Watumwa wote wawili walipata pongezi sawa, kwa kuwa wote wawili walifanya kazi kwa nafsi yote kwa bwana-mkubwa wao. Sote twaweza kujifunza kwa hayo.
-
-
Ni Nini Hukuchochea Kumtumikia Mungu?Mnara wa Mlinzi—1995 | Juni 15
-
-
20. Yehova huonaje vizuizi vyetu?
20 Yehova atazamia kila mmoja wetu kumpenda kwa nguvu zetu zote, lakini inachangamsha moyo kama nini kwamba “yeye anatujua umbo letu, na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi”! (Zaburi 103:14) Mithali 21:2 lasema kwamba “BWANA huipima mioyo”—si tarakimu. Yeye huelewa vizuizi vyovyote ambavyo hatuwezi kudhibiti, viwe vya kifedha, kimwili, kihisia-moyo, au vingine. (Isaya 63:9) Na wakati uo huo, anatutarajia tutumie kikamili mali zote ambazo huenda tunazo. Yehova ni mkamilifu, lakini anaposhughulika na waabudu wake wasiokamilika, yeye hawatazamii kuwa wakamilifu. Yeye ni mwenye kukubali sababu katika shughuli zake na asiyepitisha kiasi kwa matazamio yake.
-