-
Jifunze Kutokana na Mfano wa TalantaMnara wa Mlinzi—2015 | Machi 15
-
-
4, 5. Yule mtu, au bwana, anafananisha nani, na talanta halisi ina thamani gani?
4 Soma Mathayo 25:14-30. Kwa muda mrefu, machapisho yetu yameeleza kwamba mtu, au bwana, anayetajwa katika mfano huo ni Yesu na alisafiri ng’ambo alipopanda kwenda mbinguni mwaka wa 33 W.K. Katika mfano mwingine unaolingana na huo, Yesu anafunua kusudi lake la kusafiri ng’ambo, yaani, alisafiri “ili ajipatie mamlaka ya kifalme kwa ajili yake mwenyewe.” (Luka 19:12) Yesu hakupata mamlaka kamili ya Ufalme mara tu baada ya kurudi mbinguni.b Badala yake, ‘aliketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu, tangu wakati huo na kuendelea akingojea mpaka adui zake wawekwe kuwa kiti cha miguu yake.’—Ebr. 10:12, 13.
-
-
Jifunze Kutokana na Mfano wa TalantaMnara wa Mlinzi—2015 | Machi 15
-
-
d Baada ya mitume kufa, Shetani alianzisha uasi-imani ambao ulisitawi kwa karne nyingi. Katika kipindi hicho, kazi ya kufanya wanafunzi wa kweli wa Kristo ilifanywa kwa kiwango kidogo sana. Lakini hali hiyo ingebadilika “wakati wa mavuno,” yaani, siku za mwisho. (Mt. 13:24-30, 36-43) Tazama Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 2013, ukurasa wa 9-12.
-
-
Jifunze Kutokana na Mfano wa TalantaMnara wa Mlinzi—2015 | Machi 15
-
-
8. Bwana alitarajia nini licha ya kwamba kila mtumwa alipokea idadi tofauti ya talanta?
8 Katika mfano wa talanta, bwana alimpa mtumwa mmoja talanta tano, mwingine mbili, na mwingine moja tu. (Mt. 25:15) Ingawa kila mtumwa alipokea idadi tofauti ya talanta, bwana alitarajia kwamba wote wangekuwa na bidii katika kuzitumia talanta hizo, yaani, wangefanya yote wawezayo katika huduma. (Mt. 22:37; Kol. 3:23) Katika karne ya kwanza, kuanzia Pentekoste ya 33 W.K., wafuasi wa Kristo walianza kufanya biashara kwa kutumia talanta hizo. Kitabu cha Biblia cha Matendo kinaonyesha waziwazi bidii yao katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi.d—Mdo. 6:7; 12:24; 19:20.
KUTUMIA ZILE TALANTA KUFANYA BIASHARA KATIKA SIKU ZA MWISHO
9. (a) Wale watumwa wawili waaminifu walifanya nini na zile talanta, na hilo linaonyesha nini? (b) “Kondoo wengine” wanatimiza sehemu gani?
9 Katika siku za mwisho, hasa kuanzia mwaka wa 1919 na kuendelea, watumwa waaminifu wa Kristo waliotiwa mafuta ambao wangali duniani wamekuwa wakifanya biashara kwa kutumia talanta za Bwana. Kama wale watumwa wawili wa kwanza, ndugu na dada watiwa-mafuta wametumia kile walicho nacho kufanya yote wawezayo. Hakuna haja ya kukisia-kisia ni nani aliyepewa talanta tano na ni nani aliyepewa mbili. Katika mfano huo, watumwa wote wawili walikuwa na bidii ileile kwa kuwa walipata mara mbili zaidi ya talanta walizopewa na bwana wao. Wakristo wenye tumaini la kuishi duniani wanatimiza sehemu gani? Wanatimiza sehemu muhimu sana! Mfano wa Yesu wa kondoo na mbuzi unatufundisha kwamba wale walio na tumaini la kuishi duniani wana pendeleo la kuwaunga mkono kwa ushikamanifu ndugu za Yesu watiwa-mafuta katika kazi ya kuhubiri na kufundisha. Katika siku hizi za mwisho zilizo ngumu, vikundi vyote viwili vinashirikiana kwa bidii kama “kundi moja” katika kazi ya kufanya wanafunzi.—Yoh. 10:16.
10. Ni sehemu gani iliyo muhimu sana ya ile ishara ya kuwapo kwa Yesu?
10 Bwana anatarajia wafuasi wake wote wafanye wanafunzi zaidi. Kama ilivyotajwa awali, bila shaka wanafunzi wake waaminifu wa karne ya kwanza waliongeza mali zake. Namna gani katika siku hizi za mwisho wakati ambapo mfano wa talanta unatimizwa? Watumishi waaminifu wenye bidii wa Yesu wamefanya kazi kubwa zaidi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi katika historia. Kwa sababu ya jitihada zao, mamia ya maelfu ya wanafunzi wapya wanajiunga na watangazaji wa Ufalme kila mwaka. Hilo limefanya kazi ya kuhubiri na kufundisha kuwa sehemu muhimu sana ya ile ishara ya kuwapo kwa Yesu katika mamlaka ya Ufalme. Kwa hakika, Bwana wao anafurahi sana!
Kristo amewakabidhi watumishi wake kazi muhimu sana ya kuhubiri (Tazama fungu la 10)
-