-
Kuishiriki “Furaha” ya “Mwana-Mfalme wa Amani”Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
-
-
2. (a) Kwa habari ya Yesu, safari ya kwenda ng’ambo ya yule mtu tajiri ilifananisha nini, na alikwenda kwa nani? (b) Bwana-Mkubwa alirudi akiwa na nini?
2 Kwa kuwa yule mtu tajiri katika huo mfano anafananisha Yesu Kristo, kusafiri kwa mtu huyo kwenda ng’ambo kwa safari ndefu kunafananisha Yesu akienda kwenye Chanzo cha ile furaha ya pekee aliyokuwa akitazamia. Kwa hiyo, yeye alienda kwa nani? Waebrania 12:2 hutuambia: “Tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili [mti wa mateso] na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.” Ndiyo, kweli kweli, Yehova Mungu ndiye Chanzo cha furaha hiyo. Ni kwake alikokwenda Yesu, akaacha wanafunzi wake waaminifu hapa duniani wakiwa wamekabidhiwa “talanta” zake. Yule Bwana-Mkubwa alirudi akiwa na mambo “mengi” ambayo hakuwa nayo wakati alipokabidhi watumwa wake watatu zile talanta nane za fedha. Mfano wa mapema uliotolewa na Yesu, ule mfano wa “mafungu kumi ya fedha,” unaonyesha waziwazi kwamba kile alichorudi nacho kilikuwa ni “ufalme.”—Luka 19:12-15.
-
-
Kuishiriki “Furaha” ya “Mwana-Mfalme wa Amani”Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
-
-
4. Baada ya kutawazwa akiwa Mfalme, ni kwa sababu gani Yesu Kristo alikuwa na msingi wa pekee wa kualika “watumwa” wake waaminifu kwenye hali yenye furaha?
4 Basi, ikiwa, ilikuwa pindi yenye furaha alipojitoa tu mwenyewe kwa wakazi wa Yerusalemu, akiwa ndiye mpakwa-mafuta kwa roho ya Yehova kwa ajili ya umaliki, ilikuwa hivyo kwa kadiri kubwa jinsi gani zaidi alipotawazwa kweli kweli awe Mfalme mwishoni mwa Nyakati za Mataifa mwaka wa 1914? Ilikuwa pindi yenye furaha sana kwake. Ndipo, kweli kweli, alipoingia katika furaha asiyopata kuwa nayo kamwe wakati uliotangulia. Kwa hiyo wakati wa kufanya hesabu, angeweza kuwaambia wale wanafunzi ambao aliwahukumu kuwa ‘wema na waaminifu’ hivi: “Ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.” (Mathayo 25:21) Sasa kukawa na furaha mpya ambayo katika hiyo “watumwa” wake waliokubaliwa wangeweza kushiriki. Ni thawabu iliyoje!
5. (a) Mtume Paulo alikuwa ‘balozi’ kwa ajili ya Kristo wakati hali ya mambo ilikuwaje? (b) Lakini leo mabaki ya wapakwa mafuta ni “mabalozi” kwa ajili ya Kristo baada ya matukio gani?
5 Mwaka wa 1919 wanafunzi waliopakwa mafuta wa Mfalme anayetawala, Yesu Kristo, waliingia katika hali inayokubaliwa, nayo ilifuatana na furaha kuu kwa upande wao. Karne kumi na tisa mapema mtume Paulo aliwaandikia waamini wenzake kuwaambia juu ya cheo chao kilichotukuka: “Kwa hiyo sisi tu mabalozi badala ya Kristo.” (2 Wakorintho 5:20, NW) Hilo liliandikwa wakati Yesu alikuwa angali mrithi tu akionekana kuwa na tazamio la kuupokea ule “ufalme wa mbinguni.” (Mathayo 25:1) Kwa hiyo, basi, yeye alihitaji kuketi katika mkono wa kuume wa Mungu angojee hapo ile siku ya kuanza kutawala. Lakini sasa, tangu 1919, wale mabaki waliokubaliwa wamekuwa “mabalozi” waliopelekwa na Yule Mfalme ambaye kwa kweli anatawala. (Waebrania 10:12, 13) Fikira za Wanafunzi wa Biblia wa Kimataifa sana sana zilivutwa kwenye uhakika huo wakati wa mkusanyiko huko Seda Pointi, Ohaiyo, mwaka wa 1922.
-