-
Kuwaunga Mkono kwa Ushikamanifu Ndugu za KristoMnara wa Mlinzi—2015 | Machi 15
-
-
4 Katika mwaka wa 1881, gazeti la Zion’s Watch Tower lilimtambulisha Yesu kuwa “Mwana wa binadamu,” ambaye pia anaitwa “Mfalme.” Wanafunzi wa awali wa Biblia walielewa kwamba maneno “ndugu zangu” yanawahusu wale watakaotawala na Kristo, na pia wanadamu wote baada ya kurudishwa kwenye ukamilifu duniani. Walifikiri kwamba kondoo watatenganishwa na mbuzi wakati wa ile Miaka Elfu Moja ya Utawala wa Kristo. Na waliamini kwamba watu watahesabiwa kuwa kondoo kwa sababu waliishi kupatana na sheria ya Mungu ya upendo.
5. Uelewaji wetu uliboreshwaje katika miaka ya 1920?
5 Mwanzoni mwa miaka ya 1920, Yehova aliwasaidia watu wake kuboresha uelewaji wao kuhusu mfano huo. Gazeti Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 1923, lilithibitisha kwamba Yesu ndiye “Mwana wa binadamu.” Hata hivyo, gazeti hilo lilitaja sababu za Kimaandiko ambazo ziliwatambulisha ndugu za Kristo kuwa ni wale tu ambao wangetawala naye mbinguni, na pia lilisema kwamba kondoo ni wale wanaotumaini kuishi duniani chini ya utawala wa Ufalme wa Kristo. Vipi kuhusu wakati wa kutenganisha kondoo na mbuzi? Kulingana na makala hiyo, wale walio na tumaini la kuishi duniani hawangeweza kuwasaidia au kuwapuuza ndugu za Kristo wakati wa Utawala wake wa Miaka Elfu Moja, kwa sababu ndugu za Kristo wangekuwa mbinguni wakitawala naye wakati huo. Kwa hiyo, kondoo wangetenganishwa na mbuzi kabla ya Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu Moja. Makala hiyo ilisema kwamba sababu ya watu kuhesabiwa kuwa kondoo ni kukiri kwamba Yesu ni Bwana, na kutumaini kwamba Ufalme utaleta hali bora.
-
-
Kuwaunga Mkono kwa Ushikamanifu Ndugu za KristoMnara wa Mlinzi—2015 | Machi 15
-
-
7. Leo tunaelewa vizuri mfano gani?
7 Leo, tunaelewa vizuri maana ya mfano wa kondoo na mbuzi. Kuhusu utambulisho wa wale wanaotajwa katika mfano huo, tunajua kwamba Yesu ndiye “Mwana wa binadamu,” au Mfalme. Wale anaowaita “ndugu zangu” ni wanaume na wanawake watiwa-mafuta watakaotawala na Kristo mbinguni. (Rom. 8:16, 17) “Kondoo” na “mbuzi” wanafananisha watu wa mataifa yote. Watu hao hawajatiwa mafuta kwa roho takatifu. Namna gani kuhusu wakati wa hukumu? Hukumu hiyo itatekelezwa kabla tu ya kumalizika kwa dhiki kuu itakayoanza hivi karibuni. Na watu watahukumiwa kuwa kondoo au mbuzi kwa sababu gani? Matokeo yanategemea jinsi ambavyo wamewatendea ndugu watiwa-mafuta wa Kristo walio duniani. Kwa kuwa mwisho wa mfumo huu unakaribia sana, tunamshukuru Yehova kwa kuangaza hatua kwa hatua nuru kuhusu mfano huo na mifano mingine inayotajwa katika Mathayo sura ya 24 na 25.
-
-
Kuwaunga Mkono kwa Ushikamanifu Ndugu za KristoMnara wa Mlinzi—2015 | Machi 15
-
-
9 Kwanza, kumbuka kwamba Yesu anatumia mfano kufundisha. Bila shaka, hazungumzii kutenganishwa kwa kondoo na mbuzi halisi. Vivyo hivyo, hamaanishi kwamba kila mtu anayeonwa kuwa kondoo ni lazima amlishe, amvishe, amtunze, au kumtembelea kihalisi gerezani mmoja wa ndugu za Yesu. Badala yake, anatumia mfano kueleza mtazamo wa watu walio kama kondoo kuelekea ndugu zake. Anawaita “waadilifu” kwa sababu wanatambua kwamba Kristo ana kikundi cha ndugu watiwa-mafuta ambao wako duniani, na kondoo hao huwaunga mkono kwa ushikamanifu watiwa-mafuta katika siku hizi za mwisho ambazo ni hatari.—Mt. 10:40-42; 25:40, 46; 2 Tim. 3:1-5.
10. Kondoo wanaweza kuwaonyeshaje fadhili ndugu za Kristo?
10 Pili, fikiria muktadha wa maneno ya Yesu. Anazungumzia ishara ya kuwapo kwake na ya umalizio wa mfumo wa mambo. (Mt. 24:3) Mwanzoni mwa mazungumzo yake, Yesu alionyesha kuwa ishara hiyo ingetia ndani kazi ya pekee sana. Alisema kwamba habari njema ya Ufalme “itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa.” (Mt. 24:14) Kabla tu ya kuzungumza kuhusu kondoo na mbuzi, alisimulia mfano wa talanta. Kama ilivyoelezwa katika makala iliyotangulia, Yesu alitumia mfano huo kukazia kwamba lazima wanafunzi wake waliotiwa mafuta kwa roho, yaani, “ndugu” zake, wahubiri kwa bidii. Hata hivyo, idadi ndogo ya watiwa-mafuta ambao wangali duniani wakati wa kuwapo kwa Yesu wana kazi kubwa sana ya kuhubiri “kwa mataifa yote” kabla ya mwisho kuja. Mfano wa kondoo na mbuzi unaonyesha kwamba watiwa-mafuta wangesaidiwa kuhubiri. Kwa hiyo, njia moja ya msingi ambayo wale wanaoonwa kuwa kondoo wanawaonyesha fadhili ndugu za Kristo ni kuwaunga mkono katika kazi ya kuhubiri. Hata hivyo, kuwaunga mkono kunahusisha nini? Je, kunahusisha tu kuwasaidia kifedha na kuwatia moyo, au mengi zaidi yanahusika?
-