Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kubaki Tukiwa Tumejipanga Kitengenezo Ili Tuokoke Kuingia Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Septemba 1
    • 8. Kwa kufunga unabii wake kuhusu kuwapo kwake, Yesu alitoa kielezi gani, nayo tarehe ya Juni 1, 1935, ilikuwaje ya maana kwa habari ya kukielewa?

      8 Kulingana na Gospeli ya Mathayo, Yesu alifunga unabii wake kuhusu ishara ya kuwapo kwake kwa kielezi. Kielezi hicho ambacho kwa kawaida huitwa mfano wa kondoo na mbuzi, kinahusika sasa, wakati wa umalizio wa mfumo huu wa mambo, ulioanza mwishoni mwa Nyakati za Wasio Wayahudi katika 1914. (Mathayo 25:31-46) Tarehe ya Jumamosi, Juni 1, 1935, ilikuwa ya maana kwa habari ya kuelewa utambulishi wa kondoo kuwa washiriki wa umati mkubwa. Siku hiyo, kwenye mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika Washington, D.C., watu mmoja mmoja 840 walibatizwa kuonyesha wakfu wao [ ] kwa Yehova Mungu kupitia Yesu Kristo. Walio wengi wa hao walichukua hatua hii kwa kuuitikia haraka mhadhara uliotolewa na J. F. Rutherford juu ya Ufunuo 7:9-17. Ilikuwa tamaa yao kuwa sehemu ya umati mkubwa wa kondoo wengine wa Mchungaji Mwema, wakiwa na fursa ya kuokoka dhiki kubwa inayokuja na kuwa hai kuupita mwisho wa mfumo huu wa mambo na kuingia katika Utawala wa Mileani wa Mchungaji-Mfalme, Yesu Kristo. Hatimaye, wanafikia uhai wa milele katika dunia paradiso.—Mathayo 25:46; Luka 23:43.

      9. Kwa nini kondoo wanaalikwa warithi ‘ufalme waliowekewa tayari,’ na ni kwa njia gani wamo katika hali nzuri zaidi kuwatendea mema ndugu za Mfalme?

      9 Kwa nini watu hawa wa aina ya kondoo waalikwa ‘waurithi ufalme waliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu’? Mfalme awaambia kwamba ni kwa sababu wamewatendea “ndugu” zake mema, na kwa sababu hiyo walimtendea yeye. Kwa usemi “ndugu,” Mfalme anamaanisha mabaki wa ndugu zake wa kiroho ambao wangali duniani katika umalizio huu wa mfumo wa mambo. Wakiisha kuwa kundi moja na akina ndugu wa Mchungaji-Mfalme, Yesu Kristo, wangeshirikiana kwa ukaribu sana iwezekanavyo pamoja na mabaki wa hao na kwa hiyo wangekuwa katika hali nzuri kabisa ya kuwatendea mema. Hata katika njia za kimwili, wangewasaidia ndugu za Yesu kuhubiri ulimwenguni pote ujumbe wa Ufalme uliosimamishwa kabla mwisho haujaja. Kwa sababu hii, kondoo wangehazini pendeleo lao la kuwa wamepangwa kitengenezo pamoja na mabaki wakiwa kundi moja la Mchungaji mmoja.

  • Kubaki Tukiwa Tumejipanga Kitengenezo Ili Tuokoke Kuingia Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Septemba 1
    • 11. Kondoo wanaonyeshaje kwamba wao wanatetea Ufalme, na kwa sababu ya hilo, ni baraka gani ambayo ni yao?

      11 Kwa kutofautiana na mbuzi wa mfano, watu wa aina ya kondoo wanaonyesha kwamba wanatetea Ufalme waziwazi. Jinsi gani? Kwa vitendo, si maneno matupu tu. Kwa sababu ya kutoonekana kwa Mfalme katika mbingu, hawawezi kumtendea mema moja kwa moja kwa kuunga mkono Ufalme wake. Kwa hiyo wanawatendea mema ndugu zake wa kiroho ambao bado wako duniani. Ijapokuwa hilo linatokeza chuki, upinzani, na mnyanyaso kutoka kwa mbuzi, kwa sababu ya huko kutenda mema, kondoo wanaambiwa na Mfalme kwamba ndio ‘waliobarikiwa na Baba yake.’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki