-
“Tazama, Mtu Huyu!”Mnara wa Mlinzi—1991 | Januari 1
-
-
Hivyo basi, kulingana na madai yao—naye akitaka kufurahisha umati huo kuliko kufanya analojua kuwa haki—Pilato anawafungulia Baraba. Anachukua Yesu na kuagiza avuliwe mavazi halafu apigwe mijeledi. Huku hakukuwa kupiga viboko vya kawaida. The Journal of the American Medical Association linaeleza zoea la Kiroma la kupiga mijeledi:
“Chombo cha kawaida kilikuwa kiboko kifupi (flagramu au flagelamu) chenye kamba kadhaa moja moja za ngozi-kavu au zilizosokotwa zikiwa na marefu mbalimbali, ambamo mipira midogo ya chuma au vipande vyenye ncha kali vya mifupa ya kondoo vilifungwa kwa kuachana. . . . Askari Waroma walipopiga-piga mgongo wa mfungwa kwa nguvu kamili, ile mipira ya chuma ingesababisha michubuo ya kina kirefu, na zile kamba za ngozi-kavu na mifupa ya kondoo zingekata ndani ya ngozi na sehemu zilizo chini ya ngozi ya mwili. Halafu, kupigwa mijeledi kulipoendelea, miraruko ya ngozi ingeingia chini ya nyuzi za mnofu chini kwenye mifupa ya mwili na kutokeza nyuzinyuzi zenye kuning’inia za mnofu wenye kutoka damu.”
-
-
“Tazama, Mtu Huyu!”Mnara wa Mlinzi—1991 | Januari 1
-
-
Ingawa amechubuliwa na kutwangwa, hapa amesimama mtu mwenye kutokeza zaidi katika historia yote, kwa kweli binadamu wa kutokeza zaidi aliyepata kuishi! Ndiyo, Yesu anaonyesha fahari ya unyamavu na utulivu unaoonyesha ukuu ambao hata Pilato analazimika kuukubali wazi, kwa maana inaonekana maneno yake ni mchanganyiko wa heshima na huruma pia. Yohana 18:39–19:5; Mathayo 27:15-17, 20-30; Marko 15:6-19; Luka 23:18-25.
-