Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Kwa Jina la Roho Takatifu’
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Februari 1
    • ‘Kwa Jina la Roho Takatifu’

      “Basi enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la . . . Roho Mtakatifu [roho takatifu, NW].”—MATHAYO 28:19.

      1. Yohana Mbatizaji alitumia usemi gani mpya kuhusu roho takatifu?

      KATIKA mwaka wa 29 wa Wakati wa Kawaida wetu, Yohana Mbatizaji alikuwa mwenye shughuli katika Israeli akimtayarishia Mesiya njia, na katika huduma yake, alitangaza jambo jipya juu ya roho takatifu. Bila shaka, Wayahudi tayari walijua yale ambayo Maandiko ya Kiebrania yalisema juu ya roho. Lakini, huenda ikawa walishangaa wakati Yohana aliposema hivi: “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu . . . atawabatiza kwa Roho Mtakatifu [roho takatifu, NW].” (Mathayo 3:11) ‘Ubatizo wa roho takatifu’ ulikuwa usemi mpya kwao.

      2. Yesu alitanguliza usemi gani mpya uliohusisha roho takatifu?

      2 Yule ambaye angekuja alikuwa Yesu. Katika maisha yake ya kidunia, Yesu kwa kweli hakubatiza mtu yeyote kwa roho takatifu, ingawa mara nyingi alisema juu ya roho. Isitoshe, baada ya ufufuo wake, alirejezea roho takatifu katika njia nyingine mpya. Aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu [roho takatifu, NW].” (Mathayo 28:19) Maneno “kwa jina la” humaanisha “kwa utambuzi wa.” Ubatizo wa maji kwa utambuzi wa Baba, Mwana, na roho takatifu ungekuwa tofauti vilevile na ubatizo kwa roho takatifu. Huo pia ulikuwa usemi mpya uliohusisha roho takatifu.

  • ‘Kwa Jina la Roho Takatifu’
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Februari 1
    • Kubatizwa ‘kwa Jina la . . . Roho Takatifu’

      5, 6. Batizo za kwanza kwa roho takatifu ziliongozaje kwenye batizo za maji?

      5 Lakini vipi kuhusu ubatizo wa maji ulioahidiwa kwa jina la Baba, na Mwana, na roho takatifu? Wale wanafunzi wa kwanza waliobatizwa kwa roho hawakupitia ubatizo wa maji wa jinsi hiyo. Walikuwa tayari wamepokea ubatizo wa Yohana, na kwa kuwa huo ulikubalika kwa Yehova katika wakati huo hasa, hawakuhitaji wabatizwe upya. Lakini katika Pentekoste 33 W.K., umati mkubwa wa nafsi ulipokea ubatizo huo mpya wa maji. Hilo lilitukiaje?

      6 Ubatizo kwa roho takatifu wa wale 120 ulikuwa umeandama na sauti kubwa iliyovuta makutano ya watu. Hao walishangaa kusikia wanafunzi wakisema katika ndimi, yaani, lugha geni zenye kueleweka na wale waliokuwako. Mtume Petro alieleza kwamba muujiza huo ulikuwa ushuhuda kwamba roho ya Mungu ilikuwa imemiminwa na Yesu, aliyekuwa amefufuliwa kutoka wafu na sasa alikuwa akiketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu mbinguni. Petro aliwatia moyo wasikilizaji wake hivi: “Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha [mliyemtundika, NW] kuwa Bwana na Kristo.” Kisha akamalizia kwa kusema hivi: “Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu [roho takatifu, NW].” Nafsi zapata 3,000 ziliitikia.—Matendo 2:36, 38, 41.

      7. Wale 3,000 waliobatizwa katika Pentekoste 33 W.K. walibatizwaje kwa jina la Baba, na Mwana, na roho takatifu?

      7 Je! yaweza kusemwa kwamba hao walibatizwa kwa jina la (kwa utambuzi wa) Baba, Mwana, na roho takatifu? Naam, Ingawa Petro hakuwa amewaambia wabatizwe kwa jina la Baba, walikuwa tayari wamemtambua Yehova kuwa Bwana Mwenye Enzi Kuu, kwa kuwa walikuwa Wayahudi wa kiasili, washiriki wa taifa lililojiweka wakfu Kwake. Petro alikuwa amesema hivi: ‘Mkabatizwe kwa jina la Mwana.’ Kwa hiyo ubatizo wao ulionyesha kumtambua kwao Yesu Kristo kuwa Bwana na Kristo. Sasa walikuwa wanafunzi wake na walikubali kwamba kutoka wakati huo msamaha wa dhambi ulikuwa kupitia yeye. Mwishowe, ubatizo huo ulikuwa kwa utambuzi wa roho takatifu, na huo ulipatwa kwa kuitikia ile ahadi kwamba wangepokea roho ikiwa zawadi ya bure.

      8. (a) Pamoja na ubatizo wa maji, Wakristo wapakwa-mafuta wamepokea ubatizo gani mwingine? (b) Ni nani zaidi ya wale 144,000 wanaopokea ubatizo wa maji kwa jina la roho takatifu?

      8 Wale waliobatizwa majini siku ya Pentekoste 33 W.K. walibatizwa kwa roho pia, wakipakwa mafuta kuwa wafalme na makuhani wa wakati ujao katika Ufalme wa kimbingu. Kulingana na kitabu cha Ufunuo, kuna 144,000 tu wa hao. Kwa hiyo wale wanaobatizwa kwa roho takatifu na hatimaye ‘kutiwa muhuri’ wakiwa warithi wa Ufalme wanapata kuwa 144,000 tu. (Ufunuo 7:4; 14:1) Hata hivyo, wanafunzi wote wapya—tumaini lao liwe ni nini—wanabatizwa katika maji kwa jina la Baba, na Mwana, na roho takatifu. (Mathayo 28:19, 20) Basi, ubatizo kwa jina la roho takatifu unadokeza nini kwa Wakristo wote, kama ni wa “kundi dogo” au ni wa “kondoo wengine”? (Luka 12:32; Yohana 10:16) Kabla ya kujibu hilo, acheni tuangalie utendaji fulani-fulani wa roho katika enzi ya Kikristo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki