Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tunapaswa Kuwatendea Wengine Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Mei 15
    • 12. (a) Yesu alisema nini kuhusu nuru ya kiroho? (b) Tunaweza kuacha nuru yetu iangaze jinsi gani?

      12 Tunawatendea watu kwa njia bora zaidi tunapowasaidia kupata nuru ya kiroho kutoka kwa Mungu. (Zab. 43:3) Yesu aliwaambia wanafunzi wake kwamba walikuwa “nuru ya ulimwengu” naye aliwahimiza waache nuru yao iangaze ili watu waweze kuona ‘matendo yao mazuri’ kuelekea wengine. Kwa kufanya hivyo, wangeangaza nuru ya kiroho “mbele ya watu,” au kwa faida ya wanadamu. (Soma Mathayo 5:14-16.) Leo, tunaacha nuru yetu iangaze kwa kuwatendea mema majirani wetu na kushiriki katika kazi ya kuhubiri habari njema “katika ulimwengu wote,” yaani, “katika mataifa yote.” (Mt. 26:13; Marko 13:10) Tuna pendeleo kubwa kama nini!

  • Tunapaswa Kuwatendea Wengine Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Mei 15
    • 14. (a) Eleza jinsi taa za karne ya kwanza zilivyokuwa. (b) Kutoficha nuru ya kiroho chini ya “kikapu cha kupimia” kunamaanisha nini?

      14 Yesu alisema kuhusu kuwasha taa na kuiweka, si chini ya kikapu, bali juu ya kinara cha taa ili iwaangazie watu wote walio ndani ya nyumba. Katika karne ya kwanza, kwa kawaida taa ilikuwa chombo cha udongo chenye utambi ambao ulivuta mafuta (kwa kawaida mafuta ya zeituni) ili taa hiyo iendelee kuwaka. Mara nyingi iliwekwa juu ya kinara cha mbao au cha chuma ili ‘iwaangazie watu wote waliomo ndani ya nyumba.’ Watu hawangewasha taa na kuiweka chini ya “kikapu cha kupimia,” chombo kikubwa ambacho kingeweza kuchukua lita tisa hivi. Yesu hakutaka wanafunzi wake wafiche nuru yao ya kiroho chini ya kikapu cha kupimia cha mfano. Kwa hiyo, tunapaswa kuacha nuru yetu iangaze, na tusiruhusu kamwe upinzani au mateso yatufanye tufiche kweli ya Kimaandiko au kuwanyima wengine kweli hiyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki